EMBE FC

EMBE FC Built to unite and discourage drugs and substances abuse among Mbeere/Embu youths residing in Nairobi

LEO TUNAMZUNGUMZIA NAHODHA WA EMBE FC!Peter Mugendi almaarufu CHAMPEELeo zamu ni ya kiungo wetu ambaye si tu anajua kupa...
03/09/2026

LEO TUNAMZUNGUMZIA NAHODHA WA EMBE FC!

Peter Mugendi almaarufu CHAMPEE

Leo zamu ni ya kiungo wetu ambaye si tu anajua kupanga mipira, bali pia anajua kupanga watu!
Ni nahodha wa EMBE FC, mwenye ustaarabu wa hali ya juu—mpira ukipotea, hasemi “umeupoteza wapi?” Anaanza kwa kuuliza, “Tujipange upya ndugu zangu.”
Uwanjani ni mtu wa utulivu, hekima na nidhamu. Hata akikasirika, bado hasahau kuwa yeye ni nahodha…
Kiungo mahiri Nahodha mwenye heshima na Mtaalamu wa kupanga mchezo ni Mwenye ustaarabu wa kupigiwa mfano
Kwa kifupi, huyu ni nahodha ambaye anaongoza kwa miguu uwanjani na kwa busara nje ya uwanja!
EMBE FC: Heshima kwanza, mpira baadaye!

HAWA NAO NI  🔥  EMBE TO THE 🌎
02/09/2026

HAWA NAO NI 🔥 EMBE TO THE 🌎

LEO NI SIKU YA KIUNGO WA EMBE FC! JOHN NGOCILeo tunamzungumzia kiungo wetu mahiri, mtulivu na mwenye akili ya mpira. Huy...
02/09/2026

LEO NI SIKU YA KIUNGO WA EMBE FC!

JOHN NGOCI

Leo tunamzungumzia kiungo wetu mahiri, mtulivu na mwenye akili ya mpira.
Huyu ni yule mchezaji ambaye akishika mpira, anaanza kuhesabu pasi kabla hata mpinzani hajamaliza kufikiria!
Ana uwezo wa kutawala dimba, kutoa pasi za macho, kuunganisha safu na kuwatengenezea washambuliaji nafasi k**a vile anagawa chai kwa wageni.
Kwa kifupi, huyu si kiungo wa kawaida—ni benki kuu ya mipira ya EMBE FC! Ukimwachia nafasi, anachukua dimba; ukimkaba, anakupitisha na mpira unabaki unajiuliza umeenda wapi.
Kiungo wetu, fahari yetu! 🟢EMBE FC — Mpira ni wetu, dimba ni letu!

Leo tunapenda kutoa shukrani za dhati kwa Magaca FC kwa mechi nzuri ya kirafiki iliyochezwa jana. Tunawapongeza kwa nidh...
31/08/2026

Leo tunapenda kutoa shukrani za dhati kwa Magaca FC kwa mechi nzuri ya kirafiki iliyochezwa jana.
Tunawapongeza kwa nidhamu, upendo, heshima na ushirikiano mliouonyesha ndani na nje ya uwanja.
Mechi inaweza kuisha kwa sare, lakini urafiki na undugu wetu ndio ushindi mkubwa!
Asanteni Magaca FC — karibuni tena, sasa itakua ni Nairobi . mpira ni dakika 90 lakini urafiki ni wa maisha!
EMBE FC — Tunapiga, tunacheka, tunashikana!

baridi ni kali huku
30/08/2026

baridi ni kali huku

TAARIFA KUTOKA SIAKAGOTunapenda kuwafahamisha mashabiki na wapenzi wa EMBE FC kwamba tumefika salama hapa Siakago kwa aj...
30/08/2026

TAARIFA KUTOKA SIAKAGO
Tunapenda kuwafahamisha mashabiki na wapenzi wa EMBE FC kwamba tumefika salama hapa Siakago kwa ajili ya mechi yetu ya kirafiki ya leo.
Kikosi kimewasili, morali iko juu, na vijana wako tayari kuingia uwanjani kuonyesha kwamba Embe haijaja kutalii Siakago!
Leo mpira ndio utazungumza. Tupo tayari!
EMBE FC — Tumevuka mipaka, sasa ni kazi ya miguu! ⚽

28/08/2026

🔥 🥭

MSIMAMIZI WA USAFIRI – EMBE FC  DAVID NJIRU "KAREKE"Leo tunamwangazia mtu ambaye bila yeye, Embe FC inaweza kufika uwanj...
28/08/2026

MSIMAMIZI WA USAFIRI – EMBE FC
DAVID NJIRU "KAREKE"
Leo tunamwangazia mtu ambaye bila yeye, Embe FC inaweza kufika uwanjani… lakini wachezaji wakafika kwa miguu!
Huyu ndiye mkuu wa safari, mratibu wa magari na mlinzi wa ratiba za Embe FC. Ukimuuliza, “Gari iko wapi?” jibu lake huwa rahisi: “Iko njiani!”
Anajua kila gari, kila dereva na kila barabara—isipokuwa wakati mwingine anasahau kwamba mechi inaanza saa fulani!
Lakini kwa kweli, tunamshukuru kwa kuhakikisha kikosi chetu kinafika salama, kwa wakati na kwa ari ya ushindi.
Embe FC – Mpira unaanza uwanjani, lakini safari inaanza kwake!

27/08/2026

🚨 🔥

⚽ TAARIFA RASMI KUTOKA KWA EMBE FCSisi k**a EMBE FC tunayo furaha kuwafahamisha mashabiki wetu na umma kwa ujumla kuwa J...
27/08/2026

⚽ TAARIFA RASMI KUTOKA KWA EMBE FC

Sisi k**a EMBE FC tunayo furaha kuwafahamisha mashabiki wetu na umma kwa ujumla kuwa Jumapili hii tutakuwa na mechi kubwa ya kirafiki kule Siakago.
Tunaenda Siakago kwa amani, urafiki na mshik**ano… lakini mpira ukianza, urafiki unawekwa benchi kwa dakika 90!
Wachezaji wetu wamepewa maagizo wazi: mipira ipite, lakini pointi zisipite!
Tunawaomba mashabiki wetu kujitokeza kwa wingi kutupa sapoti. Wenye kelele waje na sauti, wenye vuvuzela waje na nguvu, na wenye mipango ya kutucheka wakipoteza—tafadhali msije mapema sana!
Siakago, tunakuja!
EMBE FC — Urafiki nje ya uwanja, ushindani ndani ya uwanja!

Address

Jericho
Zanzibar City

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when EMBE FC posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share

Category