28/03/2019
HUENDA IKAWA HABARI NJEMA KWA WANA YANGA
Nguvu ya wananchi imetia guu kunako migodi ya mwadui, inataka nini? Ni kuhusu top score wa tpl aliyeko kwa wachimba madini hao salim aiyee kwenda kukipiga jangwani.
Wao wanasemaje?
Aiyee ana mkataba na mwadui na kwakuwa bado ni kijana uongozi hautomruhusu aondoke ili kulinda kipaji chake.
Mwenyewe anasemaje?
Mpira ni hatua inapotokea umepiga hatua usijirudishe kwa makusudi huenda safari yako ya mafanikio ikawa inaanzia pale.
Wananchi wanasemaje?
Dogo analijua lango anahaha uwanja mzima yaani asipofunga moyo hauridhiki.
Aonywa kwa mifano ya wenzie!
Waangalie ditram nchimbi, adam salamba, mohamed rashid, boniventure kaheza, waziri junior walio kimbilia kufuata majina kwenye vilabu vikubwa.
Jamaa hayuko nyuma
Hata kwenye vilabu vidogo usipopambana utabaki kwenye orodha ya waliosajiriwa tu!
MWISHO WAKE UTAFIKA TU.