Viper Media Tanzania

Viper Media Tanzania sports news, analysis, fixtures and result

BREAKING : Shirika la Afya Duniani (WHO) limethibitisha kuwa wagonjwa 31 kati ya 38 waliothibitishwa kuambukizwa virusi ...
19/09/2025

BREAKING : Shirika la Afya Duniani (WHO) limethibitisha kuwa wagonjwa 31 kati ya 38 waliothibitishwa kuambukizwa virusi vya Ebola wamefariki dunia katika eneo la kusini mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ambako mamlaka zinaendelea kukabiliana na mlipuko mpya wa ugonjwa huo hatari.

Takwimu za hivi karibuni zinaonyesha kuwa kiwango cha vifo kimeongezeka mara mbili ikilinganishwa na wiki iliyopita, kutoka vifo 16, huku ugonjwa huo ukiendelea kusambaa kwa kasi. Kwa mujibu wa WHO, zaidi ya watu 900 waliowahi kuwa karibu na wagonjwa wamebainishwa. Hatua za utoaji wa chanjo zilianza Jumapili katika maeneo yaliyoathirika, ambapo wahudumu wa afya zaidi ya 500 pamoja na watu waliokuwa karibu na wagonjwa tayari wamepokea chanjo hiyo, jambo linalowapa kinga muhimu, amesema Dkt. Patrick Otim kutoka programu ya WHO Afrika.

Mamlaka za Congo zilitangaza rasmi mlipuko mpya wa Ebola mnamo Septemba 5 katika eneo la Bulape, mkoa wa Kasai, ulioko katikati mwa nchi karibu na mpaka wa Angola.

Wiki iliyopita, Kituo cha Afrika cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (Africa CDC) kiliripoti kuwa ugonjwa huo umeenea kutoka wilaya mbili hadi nne.

Kwa mujibu wa Sheillah Nsasiirwe, Afisa wa Dharura za Afya na Chanjo katika WHO Afrika, shehena mpya ya chanjo iliyoidhinishwa na Kundi la Kimataifa la Kuratibu Upatikanaji wa Chanjo (ICG) inatarajiwa kuwasili kuanzia Ijumaa hadi Jumapili.

“Utekelezaji wa chanjo haujakamilika kwa kasi tuliyokusudia kutokana na changamoto za upatikanaji na ucheleweshaji wa usafirishaji wa chanjo,” alisema. Maafisa wa WHO wameeleza kuwa chanjo hizo zimesafirishwa kwa mafungu madogo kwa sababu ya ukosefu wa miundombinu ya kuhifadhia chanjo katika eneo la Bulape.



TAARIFA KWA UMMAUongozi wa Simba Sports Club kwa kushirikiana na mzabuni wa jezi na vifaa vya michezo vya klabu, Kampuni...
18/09/2025

TAARIFA KWA UMMA

Uongozi wa Simba Sports Club kwa kushirikiana na mzabuni wa jezi na vifaa vya michezo vya klabu, Kampuni ya Jayrutty Investment East Africa Limited umebaini kuwepo kwa jezi feki za Simba zilizosambazwa mikoani, hususani mikoa ya Morogoro, Singida, Mwanza, na Geita. Ugunduzi huo umetokana na operesheni maalum iliyofanywa kwa msaada wa Jeshi la Polisi na tayari baadhi ya wahusika wamek**atwa kwa hatua kali za kisheria dhidi yao.

Simba inasisitiza kwamba uzalishaji, uuzaji, usambazaji na utumiaji wa jezi na bidhaa feki ambazo hazijazalishwa na Jayrutty Investment ni kosa kisheria na hatua kali za kisheria (Madai na Jinai) zitachukuliwa kwa yeyoye atakayethubutu kuzalisha, kuuza, kusambaza ama kutumia jezi na bidhaa feki kwani vitendo hivyo ni uhujumu wa wazi dhidi ya klabu.

Ulinzi mkali utakuwepo maeneo yote nchi nzima kudhibiti na kuk**ata wahusika wote na bidhaa feki.

Klabu inatoa rai kwa wanasimba na raia wote kutoshiriki katika matumizi ya bidhaa feki na mtu yeyote atakayebaini uwepo wa jezi na bidhaa feki mahala popote atoe taarifa kituo chochote cha Polisi na/ama kupiga Simu zifuatazo

1. 0752 111 181

2. 0784 128 220

3. 0742 771 311

Zawadi nono itatolewa kwa watakatoa taarifa zitakazofanikisha kuk**atwa kwa wazalishaji, wasambazaji, wauzaji na watumiaji wa jezi feki.

Imetolewa na:

Uongozi Klabu ya Simba kwa kushirikiana na Jayrutty Investment East Africa Limited. 18 Septemba, 2025.

15/08/2016

Kilimanajaro rangers fc inaendelea na maandalizi yake kwaajili ya Mashindano ya ujirani mwema tpc na Ligi ya mkoa kilimanjaro

27/07/2016

Timu ya New Generation hatimae imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Kipese Cup kwa mwaka 2016 baada ya kumfunga bingwa mtetezi timu ya Kilimanjaro Rangers FC katika mchezo wa fainal hapo jana katika dimba la ushirika

25/07/2016

Kilimanjaro Rangaers Fc itasuka dimbani hapo kesho kwenye mchezo wa fainal dhidi ya New Generation kutetea ubingwa wake wa Kipese Cup, katika Uwanja wa Ushirika kuanzia milango ya saa 9:30 alasiri wadau mashabiki na wapenzi wanakarishwa wajitokeze kwa wingi kushuhudia fainal hii kali na ya kusisimua

Wadau nao hawakuwa nyuma kutoa nasaa zao kwa vijana wa Rangers Thanx Mohamed Hussein Doctor na Kaka Proches
24/07/2016

Wadau nao hawakuwa nyuma kutoa nasaa zao kwa vijana wa Rangers Thanx Mohamed Hussein Doctor na Kaka Proches

24/07/2016

Baada ya ushindi mambo yalikua hivi

24/07/2016

K**a ulikosa baadhi ya matukio mambo yalikuwa hivi

Shukrani kwa mwlimu Msaidizi Bw. Salim Rashid Maarufu k**a Kidevu na Kiongozi Emmanuel Majigo Kwa kufanikisha kutinga fa...
24/07/2016

Shukrani kwa mwlimu Msaidizi Bw. Salim Rashid Maarufu k**a Kidevu na Kiongozi Emmanuel Majigo Kwa kufanikisha kutinga fainali ya mashindano haya

Ni furaha sanaaa...... Mabingwa wa Kipese Cup Kilimanjaro Rangers wakishangilia kwa furaha mara baada ya kutinga fainal ...
24/07/2016

Ni furaha sanaaa...... Mabingwa wa Kipese Cup Kilimanjaro Rangers wakishangilia kwa furaha mara baada ya kutinga fainal ya michuano hiyo kwa msimu wa pili mfululizo baada ya hapo jana kuifunga Reli ya Njoro kwa goli 2 - 0, Shukrani kwa magoli ya Peter William Masawe na Fadhili Adballah Kizenga

Address

Moshi
3053

Telephone

+255718365166

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Viper Media Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Viper Media Tanzania:

Share