10/08/2023
Taarifa muhimu sana 👇
Kumekua na kamtindo ka watu wakipata mpenzi au rafiki mpya na wakiwa wanataka kukutana kimwili basi huja hospitali na kutaka KUPIMA HIV kila mmoja wao kwa maana ya mwanaume na mwanamke.
Majibu yakija NEGATIVE utawaona wanavocheka na kufurahia huku mioyoni mwao wakiwa na hamasa na ari ya kukutana na mwenziwe.
Sasa ukweli ni kwamba kupima HIV pekee na kufurahia majibu ya HIV na kujiaminjsha ni FIKRA POTOFU NA UTAKUJA KUJUTA SIKU MOJA.
Ikumbukwe kwamba k**a mtu amepata maambukizi ndani ya wiki mbili kwa mfano na akaenda kupima bado ataonekana hana ilihali anao maana yuko kwenye window period.. Majibu yatakuja negative ilihali mtu ni positive,yapo magojwa mengine k**a KASWENDE,PANGUSA,MGEN,HOMA YA INI,KISONONO,HEPESI NK ambayo hata hawahangaiki nayo na yanaambukizwa kwa ngono. Usishangilie HIV negative, fikiria na magonjwa mengine pia na suala la window period...Chukua tahadhari!
Ndugu zangu mkienda hospitali pimeni na homa ya ini,kisonono,kaswende nk na kumbuka kujilinda na magonjwa ya zinaa👇
1) Acha kabisa kufanya ngono
2) Kua na mpenzi mmoja na muaminifu
3) TUMIA KONDOMU,USIMUAMINI MTU!!USIMUAMINI MTU!! VIJANA TAMBUENI KUA SIKU HIZI WATU NI WAZURI KWA NJE ILA NI BOMU NDANI,SIO KILA KING'AACHO NI DHAHABU.JILINDE ,USIDANGANYIKE NA UZURI WA NJE.
Muhimu sana,wewe unaepata ujumbe huu msaidie mwenzako kwa kumtagi ili nae aje ajifunze
...