Badilika Kifikra

Badilika Kifikra Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Badilika Kifikra, Moshi.

....... katika maisha ya kila siku mambo hayafanyiki haraka k**a tunavyotaka,, huwezi kutarajia mambo yatendeke kwa waka...
17/01/2026

....... katika maisha ya kila siku mambo hayafanyiki haraka k**a tunavyotaka,, huwezi kutarajia mambo yatendeke kwa wakati ambao wewe unatarajia yatendeke unahitaji subira.

21/03/2017

YAJUE MAMBO HAYA USIYOYAJUA KUHUSU UWEPO WAKO HAPA DUNIANI:- 1-Uko tofauti na wengine. 2-Unachokifanya wewe hakuna mwingine anayeweza kukifanya k**a unavyokifanya wewe. 3-Lengo kubwa la kuletwa hapa duniani ni kuja kufanya kitu na sio kuja kupita kutembea na kuzijua tu starehe za dunia. 4-Kuna kitu cha tofauti ndani mwako. 5-Watu wanasubiri kuona kitu kutoka kwako.

22/05/2016

K**A WEWE NI MWANAUME NA UNA TABIA HIZI ACHA KULALAMIKA NA KUSEMA WANAWAKE WANA TABIA MBAYA TATIZO NI WEWE:- _kila mwanamke unayemtaka lazima umpate hata k**a akukatae vipi._unapenda kujisifia na ulivyo navyo pindi unapotaka kuoa au unapomtaka mwanamke kimapenzi._unatafuta pesa kwa ajili ya kuja kupata mwanamke mzuri wa kuishi naye._unaamini mwanamke kuvaa nguo ndefu ni ushamba na hajui mapenzi._unapenda kuwasifia wanawake wanaova nguo fupi(min+top) kwamba wao ndio wazuri na wanayajua mapenzi.

09/05/2016

K**A ULIKUWA HAUJUI HIZI NDIO SABABU ZINAZOPELEKEA NDOA NYINGI KUVUNJIKA:- _wanandoa kushindwa kujua ni kitu gani kinashindwa kufanyika ukiwa kwenye ndoa. _wanawake wengi huolewa wakiwa bado hawako tayari kuolewa ila huolewa tu kwa sababu kuna mwanaume anataka kumuoa. _wanawake wengi huolewa wakiwa hawajui ni kwa nini wanaolewa ila wanaolewa tu kwa sababu anaona wenzake wanaolewa au wameolewa. _wanaume wengi huwa wanaoa wakiwa bado hawako tayari kuoa ila wanaoa tu kwa sababu kuna mwanamke amekutana naye barabarani akamvutia kimapenzi. _wanaume wengi huwa wanaoa wanawake wa kuja kuwatimizia haja zao pindi wanapowahitaji ila wanawake hao wanakuwa hawawapendi wanaume hao.

07/05/2016

......epuka sana kuitwa mtu mzima eti kwa sababu viungo vyako vyote mwilini vinafanya kazi au sio mlemavu wa viungo......wakati wenzako wanaitwa watu wazima kutokana na akili yao kutambua mema na mabaya.

06/05/2016

MAMBO KUMI YA KUZINGATIA KATIKA MAPENZI ILI MAPENZI YENU YADUMU:-1_kubali makosa yako.2_kutoelewana kwenu iwe mwanzo wa kuanza upya mapenzi yenu.3_usikubali kurudia makosa yako.4_muelewe vizuri mwenzi wako.5_usiwe mwepesi wa kuamini kila unachokisikia kuhusu mwenzi wako.6_peaneni uhuru katika uhusiano wenu.7_usiwe mwongeaji sana kuongelea mambo yaliyotokea kipindi cha nyuma.8_mfanyie mwenzi wako yale anayoyapenda.9_msifie mwenzi wako hata k**a hajafanya kitu kinachovutia.10_elewa maisha ni hali ya matokeo fulani baada ya kiumbe hai kuishi sehemu fulani,hivyo yanayotokea katika mapenzi yenu ni matokeo tu na sio kitu kibaya na wala sio mwisho wa mapenzi yenu.

03/05/2016

BAADA YA KUONA FAIDA YA NGUVU YA KWANZA NA YA PILI LEO TUNAENDELEA KWA KUITAZAMA NGUVU NYINGINE_ambayo ni nguvu ya mitazamo chanya_guvu hii haina tofauti sana na nguvu ya hamasa japokuwa yenyewe inaweza ikawa na nguvu zaidi kwa sababu k**a ulikuwa haujui mtazamo ndio huumba kitu na kutokea kweli kwa jinsi unavyokichukulia akili mwako,kwa mfano ukijijengea mtazamo wa kushindwa akili mwako ni lazima utafeli kweli kwa kile unachokifanya hata k**a ulikuwa na uwezo wa kulifanya jambo hilo hata kwa dakika moja tu ,kwa mfano jaribu kuchunguza baadhi ya familia hapo mtaani kwenu utakuta kuna familia ambayo huwa wana mtazamo kwamba familia yao haiwezi kuwa na mtu msomi au wanaamini kwamba umaskini walionao ni jambo ambalo walipangiwa toka enzi na mungu na kamwe haitakaa itokee mtu kutoka katika familia akanunua gari kumbe sio kweli ila ni mitazamo yao na imani ndio inawadanganya na hiyo ni dhana ambayo imeharibu ndoto nyingi sana pasipo kujua na nataka nikuambie hakuna mtu aliyeumbiwa kuwa tajiri au maskini.

02/05/2016

BAADA YA KUZIONA NGUVU KUBWA TANO AMBAZO ZINAWEZA KUTUFIKISHA KWENYE MALENGO YETU,LEO TUANGALIE FAIDA YA KUWA NA NGUVU HIZO KWA KUZIELEZEA MOJA BAADA YA NYINGINE:-leo tuanze kwa kuzielezea nguvu ya kwanza na ya pili ambazo ni nguvu ya hisia za kutaka huko tuendako na nguvu ya hamasa kutoka kwa waliofanikiwa, tuanze kwa kuilezea nguvu ya hisia za kutaka huko tuendako.1-NGUVU YA HISIA ZA KUTAKA HUKO TUENDAKO_nguvu hii mara nyingi huwa inatupa picha kamili ya mambo mazuri tutakayoyapata baada ya malengo yetu kutimia hivyo hujikuta tukiongeza juhudi na bidii mpaka malengo yetu yatimie kwa kujua mazuri yanayokuja mbele yetu.2-NGUVU YA HAMASA KUTOKA KWA WALIOFANIKIWA_nguvu hii tukiipata mara nyingi huwa inatusaidia kujiamini kwa kile tunachokifanya na kujiona tuna uwezo mkubwa sana wa kukifanya kitu hicho hata k**a kina changamoto nyingi kiasi gani na hatimaye hujikuta ndoto zetu na malengo yetu yakitimia bila kuwa na ugumu wala kizuizi chochote kutokana na hamasa tunayoipata,leo tunaishia hapo mpaka kesho tena.

Address

Moshi

Telephone

+255753801678

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Badilika Kifikra posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share