05/06/2026
π¨ UPDATE: Golikipa wa Klabu ya Simba SC, Yakoub Suleiman, amefanyiwa upasuaji wa goti baada ya kuendelea kusumbuliwa na jeraha alilolipata wakati wa AFCON 2025 nchini Morocco π²π¦.
Upasuaji huo umefanyika Ijumaa, Mei 22, 2026, katika Hospitali ya Ebrahim Haji, Dar es Salaam.
Yakoub alikuwa nje ya uwanja kwa zaidi ya miezi mitano bila kupata nafuu kabla ya hatua hiyo ya matibabu kufanyika.
Kwa sasa, atakosa michezo yote iliyosalia ya msimu huu, na pia sehemu ya mwanzo wa msimu ujao kutokana na kipindi cha kupona.