07/01/2026
KARIBU LIAM ROSENIOR
Mabingwa wa Kombe la Dunia la Vilabu la FIFA 2025, Chelsea, wamethibitisha kumteua Liam Rosenior kuwa kocha wao mkuu mpya kwa mkataba wa miaka mitano na nusu.
Rosenior mwenye umri wa miaka 41 anachukua nafasi ya Enzo Maresca, aliyeiongoza Chelsea kutwaa taji hilo la kihistoria la dunia, ambaye aliondoka klabuni hapo tarehe 1 Januari. Kabla ya kujiunga na Chelsea, Rosenior alikuwa kocha mkuu wa Strasbourg tangu Julai 2024, na awali aliwahi kuzinoa Hull City na Derby County