19/12/2025
RONALDO DE LIMA COULD DRIBBLE LIKE A WINGER AND RUN LIKE A SPRINTER, ASANTE MSELA WA BENTO RIBEIRO
Mitaa fulani Jijini Rio de Janeiro pale Brazil, Bento Ribeiro, hapo ni mitaa ya Kaskazini ya Jiji hilo, ilipewa jina jina kwa heshima ya Meya wao bwana Bento Manuel Ribeiro Carneiro Monteiro miaka ya 1910-1914
Ndio mitaa aliyotokea El Phenomeno, Ronaldo De Lima, kumradhi ni Ronaldo wa Brazil sio Ronaldo wa Ureno au Ronald aliyekuwa Rais wa zamani wa Marekani
Kuna masimulizi mengi juu ya fundi huyu, akibeba tuzo ya mchezaji bora wa FIFA mara 3, 1996,1997 & 2002 bado alibeba mchezaji bora UEFA mara mbili 1997 & 2002
Ubishani ni De Lima yupi bora wa Cruzeiro, PSV, Barca au Inter Milan, sisi hayo hatuwazi sana ila kuna mwamba mmoja kutoka Ufaransa alidai kulikuwa na De Lima wawili mmoja wa kabla ya majeruhi na mwingine wa baada ya majeruhi😀🙌
Mzee mmoja pale Kihesa Iringa anadai kuwa kwenye nafasi ya Center forward kuna watu watatu bora kuwahi kutokea, huyu De Lima, George Weah na Romario pekee 🙌
Hawa walikuja na style yao drop down to the midfield, switch pembeni kwenye flanks, vuta mabeki wa kati wakufate na chenga za maudhi sana 😀
Pale Nou Camp wale Wakatalunya na jeuri zao wakiona mnyama kaushika mpira kuanzia eneo la midfield kila shabiki anainuka, anapasua ngome kwa speed ya umeme, ndie binadamu mwenye kasi zaidi akiwa na mpira kuwahi tokea duniani, hats off Ma'men
Usiku mmoja wa fainali ya UEFA 1998, baada ya De Lima kumpita Alesandro Nesta, commentator aliishia kusema " He passed, he burnt and he humiliated Nesta!🙌... Simply he is extraterestial
Ronaldo anatumia miguu yote, anapiga faulo, mzuri kwenye aerial balls, kifupi ana kila kitu kwa ajili ya namba 9, ikiaminika ndie 9 bora zaidi kuwahi kubariki mchezo wa soka kwa hivi karibuni, kakutana na mabeki na makipa hatari wa zama zake, kumbuka 2002 dhidi ya Oliver Kahn pale Japan 🙌
He would dip the shoulders,stepped over and banged 🔥 Mzee kula tu maisha hapo Copa Cabana, wape hi Masela, Asante kwa kumbukumbu
Binafsi huku Ghetto hatukudai umetupa kila kitu🙏