09/02/2020
OFFICIAL | Mechi ya Premier League kati ya Manchester City dhidi ya West Ham siku ya hii leo Jumapili imesitishwa mara moja kwa sababu ya hali mbaya ya hewa... Pia Hali hiyo mbaya imesababisha kusitishwa kwa Mechi tano za Ligi Kuu ya Wanawake hapo Uingereza.
- Everton dhidi ya Liverpool na Arsenal v Spurs ni miongoni mwa mechi tano za Super League za wanawake zilizofutwa kuchezwa leo, pamoja na mbio za farasi huko Exeter, Southwell na Punchestown... Zaidi ya mashabiki 20,000 walitarajiwa kutazama Merseyside Derby kwa Wanawake huko huko Goodison Park.. Mechi nyingine zilizofutwa kupigwa hii leo kwa Wanawake ni Birmingham dhidi ya Brighton, Bristol City v Reading na West Ham v Manchester City.
:
✍🏻 Lakini Sheffield United dhidi ya Bournemouth jioni hii ndio mechi Pekee inayotarajia kupigwa kwenye Muendelezo wa Premier league jioni hii huku kwa Wanawake pia kutapigwa mechi moja tu Wenyeji, Manchester United dhidi ya Wakina Dada hatari wa Chelsea...