27/05/2026
Kwa tathmini ya haraka tu, Azam FC msimu huu wana defence nzuri..
Safu ya ulinzi inaundwa kuanzia kwa namba 6, full backs 2&3, center backs 4&5 pamoja na goli kipa..
Dimba lao la chini msimu huu limekuwa chini ya Himid Mao, mimi hupenda kumwita "Mzee Kigogo".
Himid anatoa darasa jinsi gani ya kucheza kwenye zone ile, anafanya kazi kubwa sana kupokonya mipira, anapiga pass kwa usahihi mkubwa na analinda vyema ukuta wake..
Kwenye full backs, imekuwa ni mwendelezo tu wa kile ambacho wamekuwa bora kwacho misimu kadhaa tangu wapandishwe senior team..
Captain Lusajo Mwaikenda mbavu ya kulia na Pascal Gaudence mbavu ya kushoto..🔥
Central defenders, bwana mdogo Twalib Nuru amekuja kutoa surprise kwa ma pro ambao tayari wana experience ya kutosha, ameaminiwa kucheza mechi nyingi ikiwemo za CAF pamoja na Fuentes Mendoza, huku Yoro Diaby, Landry Zouzou wakiingia pia mara chache kwenye kikosi.
Msimu bora kwao k**a idara ya ulinzi...
Golini pia wamekuwa wakigawana mechi, Aishi Manula, Zuberi Foba na Issa Fofana.
Wametoa mchango bora sana wakiihakikishia clean sheets 21 kwenye mechi 25 🔥
•Aishi Manula - 11 clean sheets
•Zuberi Foba - 09 clean sheets
•Issa Fofana - 01
Hili ni miongoni mwa maeneo ambayo Azam FC wako bora sana, hata kuwapo nafasi waliyopo sasa utagundua ni sare walizopata mechi za mwanzo kutokana na kukosa ufanisi wa kufunga..
Wakati huo bado Feisal na Iddi Nado hawaja waka k**a ilivyosasa..
Binafsi naona Azam FC watahitaji maboresho kidogo tu kwenye eneo hilo (ULINZI) kwaajili ya kuongeza nguvu zaidi📌