05/03/2018
TEGETE AWAPA SOMO YANGA.
Kocha john tegete amewapa majukumu nyota wa yanga, Ibrahim ajibu, Pius buswita na Papy Tshishimbi kuhakikisha wanafunga mabao mengi katika mchezo wa kesho dhidï ya Township Rollers ili kazi iwe rahisi watakapokwenda nchini Botswana.
Mchezo huo wa ligi ya mabingwa wa Africa unatarajiwa kupigwa hapo kesho kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam ikiwa ni mechïya kwanza kuwania kucheza hatua ya makundi.
Kocha Tegete amesema k**a yanga wanataka kuwatoa Township wanatakiwa kuwafunga mabao ya kutosha katika mchezo huo ili mpambano wa marudiano wasiwe na kazi nzito ugenïni.
Alisema wachezaji Ajib, Buswita, Mahadhi na Tshishimbi wanatakïwa kupambana kuhakikisha yanga wanapata mabao mengi.
"Huu mchezo ni muhimu kushinda mabao ya kutosha hakuna kingine zaidi ya hicho, washambuliaji wa yanga wanatakiwa kujua hili, K**a wakishindwa kufunga basi wajue kuwatoa hao Township itakuwa ngumu"
Hata hivyo kocha huyo aliwataka yanga wasidharau kabisa wabotswana hao badala yake wanatakiwa kucheza kwa kujituma na nidhamu kubwa uwanjani.
Alïsema katika mchezo wa kesho MASHABIKI wanatakiwa kuwa kitu kimoja kwani yanga wanawakilisha nchi kwahiyo wanatakiwa kuwashangiĺia ili kuwapa hamasa.
"Uzalendo hapa unatakiwa katika huu mchezo kwani yanga wanatuwakilisha sisi watanzania, ule ushabiki wa usimba na uyanga ukae pembeni kwanza sote tuwe kitu kimoja"
MUNGU IBARIKI TANZANIA👑👑