02/09/2026
🚨 Kiungo wa Chelsea na timu ya taifa ya Argentina, Enzo Fernández, amezua mjadala mtandaoni baada ya kauli yake kuhusu hamu aliyokuwa nayo ya kucheza katika klabu ya Manchester City.
Enzo amefunguka kuwa tangu akiwa kijana alikuwa na ndoto ya kuchezea klabu kubwa k**a Manchester City, akivutiwa na mfumo wa uchezaji pamoja na mafanikio ya timu hiyo chini ya Pep Guardiola.
"Licha ya kuipenda sana klabu hii, ukweli ni kwamba tangu nikiwa mdogo nilikuwa na ndoto ya kucheza kwenye klabu kubwa k**a Manchester City. Ni timu inayovutia sana kwa jinsi inavyocheza na mafanikio iliyonayo." — Kauli ya Enzo Fernández
Kauli hii imepokelewa kwa hisia tofauti na mashabiki wa Chelsea, ikizingatiwa kuwa alijiunga na Blues kwa ada ya rekodi ya pauni milioni 106.8 mapema mwaka 2023 akitokea Benfica.