08/06/2026
😬🌕 Nyota chipukizi wa Hispania, Lamine Yamal, amefunguka kuhusu kushindwa tuzo ya Ballon d'Or na kukiri kuwa aliamini angeibuka mshindi siku hiyo.
🗣️ Lamine alisema:
"Kwa kweli, nilidhani ningeshinda Ballon d'Or siku hiyo. Lakini ni jambo zuri kwamba Ousmane Dembélé ndiye aliyeshinda. Haikuwa wakati wangu bado kushinda tuzo hiyo."
"Bado nilikuwa kijana mdogo na huenda nisingeweza kuthamini uzito wa mafanikio hayo k**a alivyofanya Dembélé." 🫂
Lamine amesema kushindwa kwake kulimjenga zaidi binafsi na kumfanya kuwa mtu bora, huku akisisitiza kuwa amerejea akiwa na nguvu mpya.
✨ "Leo nimeinuka tena... na tutaona k**a mwaka huu ndiyo utakuwa mwaka wangu wa kushinda Ballon d'Or." 💭🏆
🔥 Je, unadhani Lamine Yamal ana nafasi ya kushinda Ballon d'Or 2026? 🤔🌟