Lady Ayshah

Lady Ayshah Business & Digital Marketing Coach
Founder – WIDBN (Women in Digital Business Network)
Je, biashara yako ipo mtandaoni lakini haiuzi?

Mimi nakusaidia ➡️content inayovutia wateja,Ads & mbinu sahihi
Mafunzo na ushaur 👇
https://wa.me/message/TAVGVSA3P4P6F1

Kagua account yako leo k**a kwenye account centre utaikuta account zaidi ya moja ziondoe tuKesi za kufungwa kwa account ...
11/06/2026

Kagua account yako leo k**a kwenye account centre utaikuta account zaidi ya moja ziondoe tu

Kesi za kufungwa kwa account zimekuwa nyingi mno na ikileta shida account moja na nyingine zinafutwa

Hakikisha kwenye account centre umeondoa account nyingine imebaki ya instagram tu

Tarehe ya kuzaliwa uliyoandika kwenye account yako iendane na ile ambayo ipo kwenye vitambulisho vyako

10/06/2026

Ukilielewa hili na kuzingatia hutoacha unachokifanya

Endelea kuonekana,endelea kusikika

Biashara inayouza na kupata wateja ni ile inayosikika na kuonekana mara kwa mara na wateja

Hisia ndizo zinazofanya mteja anunue. Usiuze bidhaa tu, uza hisia na matokeo yake
09/06/2026

Hisia ndizo zinazofanya mteja anunue.

Usiuze bidhaa tu, uza hisia na matokeo yake

Kuna muda unaweza kujikataa na kushindwa kuona nguvu yako sababu ya majeraha uliyonayo Kuna umuhimu mkubwa wa kujipa naf...
09/06/2026

Kuna muda unaweza kujikataa na kushindwa kuona nguvu yako sababu ya majeraha uliyonayo

Kuna umuhimu mkubwa wa kujipa nafasi ya kujisamehe na kutibu majeraha na maumivu yalipo moyoni na hii itatoa fursa kubwa ya kufanya vitu vikubwa kwa ufanisi

Hayo ni miongoni mwa mambo niliyotoka nayo kwenye event ya miaka 4 ya uponyaji na ushuhuda wa kitabu cha kovu la moyo kutoka kwa mwandishi bora Adv

Mwenyezi Mungu azidi kukubariki kwa kuwafanya wengi watabasam na kupata amani ya mioyo na mtu akikaa na wewe lazima afurahi na kucheka,hongera sana

08/06/2026

Hivi kuna mwanamke bado anaamini Kwa uzuri alionao unatosha kumpa maisha mazuri bila kupambana kujijenga kiuchumi
K**a upo toroka huko

Jana nilipata nafasi ya kushiriki event hii kuazimisha miaka minne ya Kitabu cha Kovu la Moyo kilichoandikwa na Adv  mia...
07/06/2026

Jana nilipata nafasi ya kushiriki event hii kuazimisha miaka minne ya Kitabu cha Kovu la Moyo kilichoandikwa na Adv miaka 4 ya uponyaji na ushuhuda

Ilikuwa zaidi ya event ilikuwa safari ya kujitafakari, kujielewa na kuanza kuruhusu uponyaji wa majeraha ambayo wengi hubeba kimya kimya

Kwa hakika, tuliingia tukiwa watu fulani, lakini tulitoka tukiwa na mtazamo mpya, matumaini mapya na nguvu mpya za kuendelea

Nimekuwa nikifanya consultation na wafanyabiashara wengi wakati mwingine biashara kutokufanya vyema sababu sio soko wala bidhaa ni mtu mwenyewe kukosa utulivu akili na hisia kwa ajili ya maumivu anayoyabeba muda mrefu

Haijalishi tumepitia changamoto gani na tunapitia nini tujipe nafasi ya kuponya maumivu ili kupata utulivu wa nafsi na akili na kutimiza ndoto na mafanikio na hiki kitabu kinakupa muongozo mzuri wa kujiponya

Kosa la wafanyabiashara wengi ni kuangalia matokeo ya biashara nyingine bila kuelewa mfumo uliowafikisha hapoMachimbo ya...
04/06/2026

Kosa la wafanyabiashara wengi ni kuangalia matokeo ya biashara nyingine bila kuelewa mfumo uliowafikisha hapo

Machimbo yana mfumo wake,biashara yako ina mfumo wake

Ukijaribu kuendesha biashara yako kwa kanuni za biashara tofauti, unaweza kujikuta unapoteza wateja na fursa za ukuaji

Jifunze kutoka kwa wengine, lakini jenga mfumo unaofaa biashara yako

Kwa sababu biashara haikui kwa kuiga kila kitu, inakua kwa kufanya maamuzi sahihi kwa mazingira yako

K**a wao huwaoni sana online usitegemee na wewe ukitumia mfumo huo ni sahihi kwako

Kabla hujataka kuiga mfumo wa mtu fulani angalia zaidi aina ya biashara yako,aina ya wateja wako,soko lako

Umewahi kusikia mfanyabiashara akisema mbona machimbo mengine hawafanyi hivi wala hawana account online na wanauza sana nami nifanye k**a wao?

Kwa wapenzi wasomaji vitabu na kupenda kujifunza hii event sio ya kukosa Hata k**a basi hujakisoma hili kitabu hii ni fu...
04/06/2026

Kwa wapenzi wasomaji vitabu na kupenda kujifunza hii event sio ya kukosa

Hata k**a basi hujakisoma hili kitabu hii ni fursa ya kuhudhuria na kujifunza mengi zaidi

Kwenye watu wengi kuna mengi ya kujifunza na fursa pia

Fursa na Yale tunayoyaomba mara nyingine huwa yapo kwenye mazungumzo ya watu ambao hatujuani nao

Hakikisha kukutana na event k**a hizi hubaki nyuma

Usipange kukosa na lipia mapema

Kwa taarifa zaidi wasiliana na Mariam Mbano

Wafanyabiashara wengi wanafanya vitu vingi kila siku wakiamini wanafanya marketingLakini mwisho wa siku mauzo hayaongeze...
03/06/2026

Wafanyabiashara wengi wanafanya vitu vingi kila siku wakiamini wanafanya marketing

Lakini mwisho wa siku mauzo hayaongezeki
Sababu ni kwamba marketing sio shughuli, marketing ni matokeo

Marketing halisi hujenga uaminifu,huonyesha thamani ya bidhaa au huduma yako,humsaidia mteja kufanya maamuzi na hubadilisha umakini wa watu kuwa mauzo

Biashara yako haihitaji followers wengi pekee, inahitaji mfumo unaoweza kubadilisha watazamaji kuwa wateja

Ni jambo gani kwenye carousel hii umekuwa ukifanya ukidhani ni marketing?

Address

Dar Es Salaam

Telephone

0679400278

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Lady Ayshah posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Lady Ayshah:

Share

Category