14/03/2020
Kusaidia wahitaji kwafaa sana lakini kusaidia bila ya kujionyesha mbele ya watu kwafaa Zaidi (rej. Mt. 6:16-18); “maana imeandikwa, unapotoa sadaka hata mkono wako wa kushoto usijue ufanyalo mkono wako wa kuume.” (Mt. 6:3). Kuwasaidia wahitaji wakati wa sikukuu kwafaa sana lakini kuwasaidia kila mara unapojaliwa chochote kwafaa zaidi. Hivyo, matendo yetu ya nje yafaa kuwa ya unyenyekevu ili yazifaidie roho zetu, tusiwe sawa na wanafiki ambao hufanya mambo yao kwa matangazo makubwa na kupenda kujulikana na kila mtu kwamba wao ndio waliotenda jambo hili ama lile (rej. Mt. 6:1). Kusoma kiaminifu Neno la Mungu na kulitafakari: K**a tulivyodokeza hapo juu, na hili ni mojawapo ya mazoezi muhimu sana ya Kiroho. Ili kuwa imara kiroho yatupasa kulisoma na kulitafakari Neno la Mungu mara kwa mara na kulielewa. Kwa kulisoma Neno la Mungu, kulitafakari na kulielewa tunapata ulinzi wa Mungu (rej. Isa. 30:12), tunapewa hekima ya kimungu (rej. Yak.1:5), tunapata faraja (rej. Zab 23:4), na mwangaza wa kiroho (rej. Zab119:18).