Kasimpya Digital

Kasimpya Digital Ukurasa huu ni Kwa ajili Habari,Michezo na matukio mbalimbali Utapata Habari zote za Ndani na Nje ya Nchi
(2)

12/06/2026

DODOMA.

Huzuni na majonzi vimetawala katika Chuo Kikuu cha St. John, jijini Dodoma Leo 12 juni 2026,wakati wa ibada ya kuaga mwili wa mwanafunzi wa mwaka wa tatu wa fani ya Afya, Rebeca James Misungwi, aliyefariki dunia baada ya kujeruhiwa katika ajali ya moto iliyotokea usiku wa kuamkia Jumapili, Juni 7, 2026, katika nyumba aliyokuwa akiishi pamoja na rafiki yake, Felister Peter Francis ambaye anaendelea na matibabu Katika hospitali ya Benjamini Mkapa.

Rebeca alifariki dunia Juni 11, 2026, katika Hospitali ya Benjamin Mkapa alipokuwa akipatiwa matibabu kutokana na majeraha aliyoyapata kwenye tukio hilo. Baada ya ibada ya kuuaga mwili wake iliyofanyika chuoni hapo, mwili umesafirishwa kuelekea mkoani Mwanza kwa ajili ya mazishi.

Akizungumza kwa niaba ya familia, kaka wa marehemu, Pascal Kapote, amesema wamepokea kwa masikitiko makubwa msiba huo na kuliomba Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini chanzo cha tukio hilo na kuhakikisha mtuhumiwa anayehusishwa na tukio hilo anachukuliwa hatua za kisheria.

"Familia inaamini kuwa haki itatendeka kupitia uchunguzi wa vyombo husika," amesema Pascal.

Aidha, amesema baada ya kuuaga mwili huo, familia inaelekea mkoani Mwanza kwa ajili ya maandalizi ya mazishi, huku akibainisha kuwa ratiba kamili ya mazishi itatangazwa mara baada ya mwili kuwasili nyumbani.

Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi wa tukio hilo ili kubaini mazingira halisi yaliyosababisha ajali hiyo ya moto.

12/06/2026

Rais Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa taasisi za kifedha kuwa wabunifu katika utoaji wa mikopo na kuacha kutegemea aina za dhamana ambazo wananchi walio wengi hawana.

12/06/2026

DODOMA, Juni 12, 2026

Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC) imetoa siku saba kwa taasisi zote zinazokusanya au kuchakata taarifa binafsi kukamilisha usajili wake, ikionya kuwa hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi ya taasisi zitakazoshindwa kutekeleza matakwa ya Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi, Sura ya 44.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi, Dkt. Emmanuel Mkilia, alisema kuwa ni marufuku kwa taasisi yoyote kukusanya au kuchakata taarifa binafsi bila kusajiliwa na Tume k**a mkusanyaji au mchakataji wa taarifa binafsi. Amesema kipindi cha mpito cha utekelezaji wa sheria kilianza Aprili 8, 2025 na kinakamilika Aprili 8, 2026, huku utekelezaji kamili wa sheria ukianza Aprili 9, 2026.

Dkt. Mkilia amesema hadi sasa zaidi ya taasisi 14,000 zimekamilisha usajili, jambo linaloonyesha mwitikio mzuri wa wadau katika kutekeleza matakwa ya sheria. Hata hivyo, alisema bado kuna baadhi ya taasisi zinazoendelea kukusanya au kuchakata taarifa binafsi bila kufuata taratibu za kisheria, hali inayoweza kuhatarisha haki ya faragha ya wananchi na kusababisha matumizi yasiyoidhinishwa ya taarifa hizo.

Kutokana na hali hiyo, Tume imezielekeza taasisi ambazo zimeanza mchakato wa usajili lakini hazijaukamilisha kufanya hivyo ndani ya siku saba kuanzia Juni 12, 2026. Aidha, taasisi ambazo bado hazijaanza usajili zimetakiwa kuanza mara moja na kuukamilisha ndani ya muda huo, huku zote zikijiandaa kwa ukaguzi wa utekelezaji wa sheria utakaofanywa na Tume.

Mbali na hilo, Tume imezitaka taasisi kuhakikisha zinaweka mifumo madhubuti ya kulinda taarifa binafsi dhidi ya matumizi yasiyoidhinishwa, upotevu au uvujishaji wa taarifa. Pia imewahimiza wananchi kufahamu haki zao za faragha na kutoa taarifa kwa Tume endapo watabaini ukiukwaji wa sheria au matumizi yasiyo halali ya taarifa zao binafsi.

Aidha, Dkt. Mkilia amesema Tume itaendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu ulinzi wa taarifa binafsi na matumizi salama ya teknolojia katika huduma za kidijitali.

11/06/2026

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), linatarajia kujenga vituo 50 vya kuchajia vyombo vya usafiri vinavyotumia umeme nchini, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuhamasisha matumizi ya nishati safi na kulinda mazingira.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kituo cha kwanza cha kuchajia vyombo vya usafiri wa umeme jijini Dodoma ,Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Lazaro Twange, amesema wananchi watapata huduma ya kuchaji magari, bajaji na vyombo vingine vya usafiri bila malipo kwa kipindi cha mwezi mmoja kuanzia siku ya uzinduzi.

Mbali na uzinduzi huo, TANESCO pia amesaini makubaliano na wadau wa majiko ya umeme yenye lengo la kuwezesha wananchi kuyapata kwa mkopo. Malipo yatafanyika kwa awamu kupitia ununuzi wa umeme wa LUKU, hatua inayolenga kuongeza matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Twange amesema Serikali imejiwekea lengo la kuhakikisha ifikapo mwaka 2034, asilimia 80 ya wananchi watakuwa wanatumia nishati safi ya kupikia. Alifafanua kuwa sekta ya umeme inatarajiwa kuchangia asilimia 20 ya lengo hilo, huku kiwango cha sasa kikiwa kimefikia asilimia 4.8.

Aidha, amesema uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali katika sekta ya umeme umeongeza uwezo wa uzalishaji hadi zaidi ya megawati 4,000. Ametaja Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere wenye thamani ya takribani shilingi trilioni 6.5 kuwa miongoni mwa miradi mikubwa iliyochangia mafanikio hayo, ukiwa na uwezo wa kuzalisha megawati 2,115.

Kuhusu mpango wa mikopo ya majiko ya umeme, Twange amesema TANESCO inalenga kuwafikia wateja milioni moja watakaonufaika na mpango huo, ambapo watarejesha mikopo ndani ya kipindi cha miaka mitatu.

Ameeleza kuwa wateja wa makundi yote wanaweza kunufaika na mpango huo, lakini kipaumbele kitatolewa kwa wamiliki wa nyumba na makazi. Aidha, mwombaji anatakiwa kuwa mteja wa TANESCO kwa angalau miezi mitatu na kuwa na kitambulisho cha NIDA

11/06/2026

DODOMA.

Serikali imependekeza kusamehe Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwenye mita janja za gesi ya kupikia (LPG Smart Meters) zinazoingizwa nchini, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia na kupunguza utegemezi wa nishati zisizo rafiki kwa mazingira.

Pendekezo hilo limewasilishwa leo bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis M***a Omar, wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2026/2027.

Akizungumza wakati wa uwasilishaji wa bajeti, Waziri Omar amesema hatua hiyo ni sehemu ya maboresho ya mfumo wa kodi yanayolenga kuongeza upatikanaji na matumizi ya teknolojia za nishati safi katika sekta ya kaya na usafiri.

Mbali na msamaha huo wa VAT kwa mita janja za gesi, Serikali imeendelea kutoa vivutio mbalimbali vya kikodi vinavyolenga kuimarisha matumizi ya nishati safi. Vivutio hivyo vinajumuisha msamaha wa VAT katika mnyororo wa uzalishaji wa Gesi Asilia Iliyoshindiliwa (CNG), vifaa vya kubadilisha magari kutoka matumizi ya mafuta kwenda gesi asilia au umeme, pamoja na malighafi zinazotumika kutengeneza mitungi ya gesi.

Hatua hizo zinaakisi dhamira ya Serikali ya kuharakisha mpito kuelekea matumizi ya nishati safi nchini kupitia sera na maboresho ya kikodi yaliyopendekezwa katika Bajeti ya mwaka wa fedha 2026/2027, kwa lengo la kuboresha afya za wananchi, kulinda mazingira na kuongeza upatikanaji wa nishati salama na nafuu

11/06/2026

Serikali imesema itaendelea kuwekeza katika ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) na uhuishaji wa Reli ya TAZARA k**a sehemu ya mkakati wa kuimarisha uchumi, biashara na usafirishaji nchini.

Akiwasilisha Bajeti ya Serikali ya mwaka 2026/27 bungeni Dodoma, Waziri wa Fedha, Balozi Khamis M***a Omar, amesema miradi hiyo itarahisisha usafirishaji wa mizigo na abiria, kuongeza fursa za uwekezaji na ajira, pamoja na kuimarisha ushindani wa Tanzania katika kuhudumia nchi jirani zisizo na bandari.

Ameeleza kuwa shilingi trilioni 1.27 katika sekta ya reli, ambapo trilioni 1.12 zimeelekezwa kwenye ujenzi wa SGR. Aidha, huduma za reli kati ya Dar es Salaam na Dodoma tayari zimeanza kutolewa.

Kwa mujibu wa Balozi Khamis M***a Omari, uwekezaji huo pamoja na miradi ya bandari, barabara na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato utaifanya Dodoma kuwa kitovu cha biashara na uchumi, huku ukiiimarisha Tanzania k**a lango muhimu la biashara katika Afrika Mashariki na Kati.

11/06/2026

Serikali imependekeza kupunguza ushuru wa forodha kutoka asilimia 25 hadi asilimia 10 kwa baadhi ya magari yanayotumia umeme katika hatua inayolenga kuhamasisha matumizi ya nishati safi na mbadala nchini.

Hatua hiyo imetangazwa leo Juni 11, 2026 bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis M***a Omar, wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2026/2027.

Waziri Omar amesema pendekezo hilo ni sehemu ya hatua za kodi zinazolenga kuchochea matumizi ya teknolojia za nishati safi katika sekta ya usafiri.

Aidha, Serikali imependekeza kutoa unafuu wa ushuru wa forodha kwenye betri za umeme zinazotumiwa na wazalishaji au waunganishaji wa magari na pikipiki za umeme pamoja na kuendelea kutoa vivutio vya kikodi kwa waunganishaji na wazalishaji wa vyombo vya moto vinavyotumia umeme na gesi.

Katika hatua nyingine, Serikali imependekeza kusamehe Kodi ya Ongezeko la Thamani kwenye vifaa vinavyotumika katika vituo vya kuchaji magari ya umeme vinavyoingizwa nchini ili kuwezesha maendeleo ya miundombinu ya nishati safi.

Mapendekezo hayo yamewasilishwa katika bajeti ya mwaka wa fedha 2026/2027 ikiwa ni sehemu ya hatua za kuhamasisha matumizi ya nishati safi na mbadala katika vyombo vya moto nchini..

11/06/2026

Serikali imeweka lengo la kuhakikisha kuwa asilimia 20 ya vyombo vya moto vinavyoingia na kutumika nchini vinakuwa vinatumia umeme, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi, kupunguza gharama za usafiri na kulinda mazingira.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Nishati, Deogratius John Ndejembi, wakati wa uzinduzi wa kituo cha kuchajia vyombo vya usafiri vinavyotumia umeme pamoja na hafla ya utiaji saini wa makubaliano ya ukopeshaji wa majiko ya umeme kati ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na wadau mbalimbali 11 Juni 2026 jijini Dodoma.

Waziri Ndejembi amesema Serikali inaamini lengo hilo linawezekana kufikiwa kutokana na mwitikio unaoendelea kuongezeka wa wananchi kutumia magari na pikipiki za umeme, ambazo zina gharama ndogo za uendeshaji na ni rafiki kwa mazingira.

Ameeleza kuwa licha ya magari ya umeme kuwa na gharama kubwa wakati wa ununuzi, matumizi yake ni nafuu kwa kuwa hayahitaji huduma za mara kwa mara k**a kubadilisha mafuta ya injini, vichujio na vipuri vingi k**a ilivyo kwa magari yanayotumia mafuta. Badala yake, mtumiaji huhitaji kuchaji umeme, kufanya usafi wa gari na kubadilisha matairi yanapoisha muda wake.

Amebainisha kuwa safari ya takribani kilomita 450 kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma kwa gari la mafuta inaweza kugharimu kati ya shilingi 250,000 na 300,000, kutegemeana na aina ya gari. Kwa upande wa gari la umeme, alisema kiasi cha shilingi 27,000 hadi 28,000 za umeme kinaweza kuliwezesha kusafiri takribani kilomita 400, hali inayowezesha mtumiaji kuokoa fedha nyingi kwa muda mrefu.

Aidha, amesema pikipiki ya umeme inaweza kusafiri hadi kilomita 1,000 kwa kutumia umeme wenye thamani ya takribani shilingi 3,000, jambo linaloonyesha faida kubwa ya kiuchumi kwa watumiaji.

Akizungumzia miundombinu, Waziri Ndejembi amesema uzinduzi wa vituo vya kuchajia vyombo vya usafiri vya umeme utaondoa changamoto kwa watumiaji na kuongeza imani kwa wawekezaji pamoja na wadau wa sekta ya usafiri wa umeme nchini.

11/06/2026

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) wamesaini makubaliano ya ushirikiano yatakayowezesha kutangazwa kwa majiko ya umeme kwa utaratibu wa kukopeshwa kwa wateja.

Makubaliano hayo yanalenga kuongeza matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini kwa kuwapa wananchi fursa ya kupata majiko ya umeme kwa urahisi zaidi.

Hafla ya utiaji saini imefanyika leo, Juni 11, 2026, jijini Dodoma, ikihusisha Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO, Mhandisi Lazaro Twange, huku ikishuhudiwa na Waziri wa Nishati, Dkt. Deogratius Ndejembi.

Mpango huo unatarajiwa kuboresha upatikanaji wa majiko ya umeme kwa wananchi, kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia, kulinda mazingira na kuchangia kuboresha afya za watumiaji.

11/06/2026

Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius J. Ndejembi (Mb.), akiwa pamoja na viongozi wengine, akikata utepe na kuweka jiwe la msingi katika uzinduzi wa Kituo cha Kuchajia Vyombo vya Usafiri Vinavyotumia Umeme katika Ofisi za Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) jijini Dodoma, leo tarehe 11 Juni, 2026.

Uzinduzi huo unaambatana na utiaji saini na uzinduzi wa miradi ya nishati safi, ikiwemo Mradi wa Ujenzi wa Vituo vya Kuchajia Vyombo vya Usafiri Vinavyotumia Umeme (EV Charging Stations) pamoja na Mpango wa Ukopeshaji wa Majiko ya Umeme kwa Wateja wa TANESCO (On-Bill Financing – OBF), uliofanyika katika Viwanja vya Mashujaa, Jamatini jijini Dodoma.

Mradi huu unalenga kuboresha maisha ya wananchi na wateja wa TANESCO kupitia upatikanaji wa nishati safi ya umeme, nafuu na yenye ufanisi katika sekta za usafirishaji na matumizi ya kupikia.

Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255622963395

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kasimpya Digital posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category