NEVES sports

NEVES sports Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from NEVES sports, Sports, Dar es Salaam.
(1)

⚽πŸ’₯𝐒𝐩𝐨𝐫𝐭𝐬 π€π§πšπ₯π²π¬π­πŸ“πŸ“²: Usipitwe na πŸ“’ Habari za nyota mbali mbali ,Updates za ligi mbalimbali, matokeo ya mechi, uchambuzi wa kina na makala kemkem🎯

πŸŒπ€π‹π‹ π€ππŽπ”π“ 𝐓𝐇𝐄 𝐋𝐀𝐓𝐄𝐒𝐓 π…πŽπŽπ“ππ€π‹π‹ π’ππŽπ‘π“π’ 𝐍𝐄𝐖𝐒
⚽

Ni winga mmoja tu duniani kwa sasa ambaye anapimwa kuwa na kiwango  cha juu kuliko Lamine Yamal.Unaweza kumtaja huyo win...
13/05/2026

Ni winga mmoja tu duniani kwa sasa ambaye anapimwa kuwa na kiwango cha juu kuliko Lamine Yamal.

Unaweza kumtaja huyo winga??πŸ€”

Ni vilabu 3 pekee pale  Premier League ambavyo havijapata kadi nyekundu hata moja mpaka kufikia sasa.Manchester City,Bri...
13/05/2026

Ni vilabu 3 pekee pale Premier League ambavyo havijapata kadi nyekundu hata moja mpaka kufikia sasa.

Manchester City,Brighton & Hove Albion na
Arsenal.

Msimu wa 2024/25, Phil Foden na Cole Palmer  kwa pamoja walizalisha  assist  10 kwenye Premier League.Lakini msimu huu m...
13/05/2026

Msimu wa 2024/25, Phil Foden na Cole Palmer kwa pamoja walizalisha assist 10 kwenye Premier League.

Lakini msimu huu mpaka sasa? Wana assist 𝙣4 tu pekee.😳

Cristiano Ronaldo bado yupo kwenye mapambano makali sana ya kushinda kiatu cha mfungaji bora  huko Saudia ila kazi ni ng...
13/05/2026

Cristiano Ronaldo bado yupo kwenye mapambano makali sana ya kushinda kiatu cha mfungaji bora huko Saudia ila kazi ni ngumu sana.

Ili Cristiano Ronaldo abebe kiatu cha mfungaji bora wa Ligi Kuu Saudi Arabia, inahitajika afunge mabao 6 au zaidi kwenye mchezo wa mwisho dhidi ya Damac.

Wakati huo huo, Ivan Toney asifunge bao lolote, na JuliΓ‘n QuiΓ±ones asifunge zaidi ya mabao 2 kwenye mechi zao zilizobaki.

Mbaya zaidi, wote Ivan Toney na QuiΓ±ones bado wamebakiza mechi mbili kila mmoja.

Huyo wa upande wa kushoto wa Ronaldo anaitwa Ali Lajami beki ambaye kwa sasa anaichezea Al Hilal, huyu jamaa kwenye mche...
13/05/2026

Huyo wa upande wa kushoto wa Ronaldo anaitwa Ali Lajami beki ambaye kwa sasa anaichezea Al Hilal, huyu jamaa kwenye mchezo wa jana aliingia dakika ya 69 kuchukua nafasi ya Hassan Altambakti.

Pamoja na makosa ya golikipa wa Al Nassr Bento ila huyu ndiyo aliyerusha ule mpira mpaka kupelekea Bento kuchanganyana na mabeki wake mpira ukaingia wavuni,kiufupi anarusha mipira sana.

Pia Ali ana pacha wake ambaye anaichezea klabu ya Al Taawoun na yeye pia ni beki na ndiyo huyo hapo upande wa kulia kwa Cristiano Ronaldo.

πŸ”΄JUST IN!!! Klabu ya Paris Saint-Germain imeanza kufanya mawasiliano na watu wa karibu wa Federico Valverde kuhusu uweze...
13/05/2026

πŸ”΄JUST IN!!! Klabu ya Paris Saint-Germain imeanza kufanya mawasiliano na watu wa karibu wa Federico Valverde kuhusu uwezekano wa kumsajili kwenye dirisha kubwa lijalo.

Via.

Kutana na David Sanchez Miralles mwenye miaka 11, mmoja wa vipaji vinavyong’aa zaidi kwenye akademi ya Real Madrid kwa s...
13/05/2026

Kutana na David Sanchez Miralles mwenye miaka 11, mmoja wa vipaji vinavyong’aa zaidi kwenye akademi ya Real Madrid kwa sasa.

Kinda huyo tayari amekamilisha zaidi ya dribbles 100+ kwenye mashindano ya LaLiga U-12, akionyesha uwezo mkubwa wa kucheza na mpira, kujiamini, na ubunifu wa hali ya juu.

Ni tishio kubwa kwenye safu ya ushambuliaji, anatengeneza nafasi kwa urahisi na kufunga mabao kwenye mechi zenye ushindani mkubwa.

Ni ishara ya nyota mkubwa wa baadaye.

Sema mwenetu  Neymar alijua kuwaibia maostadh kule SaudiaπŸ™ŒUkute haya masaibu anayokumbana nayo sasa hivi maostadh walifa...
13/05/2026

Sema mwenetu Neymar alijua kuwaibia maostadh kule SaudiaπŸ™Œ

Ukute haya masaibu anayokumbana nayo sasa hivi maostadh walifanya jambo😁

Ukiachana na mkongwe David Beckham hakuna mchezaji aliyefunga mabao mengi ya mipira ya kutenga pale ligi kuu Uingereza  ...
13/05/2026

Ukiachana na mkongwe David Beckham hakuna mchezaji aliyefunga mabao mengi ya mipira ya kutenga pale ligi kuu Uingereza kumzidi fundi π™…π™–π™’π™šπ™¨ 𝙒𝙖𝙧𝙙-π™‹π™§π™€π™¬π™¨π™š.

Huyu jamaa amefunga jumla ya mabao 17 akizidiwa na Beckham goli moja tu.

Kwasasa yuko Burnley akiwa amecheza michezo 18,hana goli hata 1 ila amebahatika kuasist goli 1 pia wameshuka daraja.

Al-Nassr wanaweza kutwaa mataji 2 ndani ya saa 24 pekee.βœ…οΈLigi: K**a Al-Hilal wakidondosha pointi dhidi ya Neom, basi Al...
13/05/2026

Al-Nassr wanaweza kutwaa mataji 2 ndani ya saa 24 pekee.

βœ…οΈLigi: K**a Al-Hilal wakidondosha pointi dhidi ya Neom, basi Al-Nassr watatangazwa rasmi mabingwa wa Saudi Pro League.

βœ…οΈFainali ya Asian Champions League 2: Al-Nassr pia wanatarajiwa kucheza dhidi ya Gamba Osaka siku hiyo hiyo.

Safari hii wakikaza wanabeba mataji ila hapa kwa Al Hilal kudondosha pointiπŸ€”

Cristiano Ronaldo alibakiwa na  sekunde 10 tu kutwaa taji lake la kwanza la ligi ndani ya miaka 6 lakini golikipa wake a...
12/05/2026

Cristiano Ronaldo alibakiwa na sekunde 10 tu kutwaa taji lake la kwanza la ligi ndani ya miaka 6 lakini golikipa wake akajifunga bao la kujifunga dakika ya 98.

Matokeo hayo yanamaanisha Al Hilal bado wako kwenye mbio za ubingwa huku ikiwa imebaki mechi moja tu kwa Al Nassr wakati Al Hilal akiwa na michezo 2 ili ligi kutamatika.

Kwa sasa Al Nassr ana pointi 83 wakati Al Hilal akiwa na pointi 78.

✍️Akikosa tena kombe la ligi awamu hii basi this man must be cursed in Saudia😭

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when NEVES sports posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to NEVES sports:

Share

Category