30/01/2026
Jeshi la Uganda limekiri kuwa wanajeshi walimk**ata kwa muda mfupi Barbara “Barbie” Kyagulanyi, mke wa kiongozi wa upinzani Robert Kyagulanyi Ssentamu maarufu k**a Bobi Wine, na baadaye kumuachilia huru, huku wakiashiria kuwa alisaidia katika jitihada za kumtafuta mumewe.
Katika chapisho kwenye mtandao wa X, Jenerali Muhoozi Kainerugaba, Kiongozi wa Jeshi la Ulinzi wa Wananchi wa Uganda, ameweka picha ya Barbie wakati wanajeshi walipochukua hatua hiyo usiku wa Januari 23 katika eneo la Magere, Wilaya ya Wakiso.
Jenerali Kainerugaba alisema: “Walimk**ata na kisha kumuachilia huru Kabobi wake, Barbie. Alikuwa msaada mkubwa katika kutupatia taarifa za mumewe.”
Hata hivyo, Jenerali Kainerugaba ameikana madai ya kudhalilishwa kwa mke huyo. Ameashiria kuwa jeshi halimdhalilishi wanawake na lengo kuu ni kumtafuta Bobi Wine, sio kuwadhalilisha wanafamilia wake.
Tukio hili linatokea katika hali ya utafutaji mkali wa Bobi Wine, ambaye amekuwa mafichoni kufuatia uchaguzi wa rais uliofanyika Januari 15, ambapo matokeo rasmi yalionyesha Rais wa sasa Yoweri Museveni kuibuka na ushindi wa muhula wa saba.