11/06/2026
DARASA HURU 💁🏾♂️
HASSAN MWAKINYO AMEPOTEZA PAMBANO RAUNDI YA 9 TKO DHIDI YA MICHEL SORO KUWANIA UBINGWA WA DUNIA IBO RAUNDI 12.
Elcapitano Maestro 🗣 kuna haja kubwa sana kwa mabondia kushikwa mkono maana sekta ya boxing ni pana sana na inahitaji uwekezaji mkubwa.
mfano...serikali ya Marekani haitoi mchango wa kifedha au ruzuku yoyote ya moja kwa moja kwa mabondia wa nchi hiyo tofauti na mataifa mengine.
lakini marekani ni kitovu cha boxing kwasababu makampuni binafsi wamewekeza sana na kuifanya boxing kuwa biashara.
Mashirika ya Kibinafsi na Hisani: Mashirika k**a vile USA Boxing Foundation huchangisha fedha kusaidia gharama za kambi, vifaa, na masomo ya boxing.
hapo utagundua kwamba boxing ni zaidi ya mazoezi na ni zaidi ya kuwa nunda.
tathmini fupi pambano la mwakinyo dhidi ya michel soro...
mwakinyo alikuwa anagombea ubingwa wa dunia IBO, na kitendo cha kuwepo kwa hilo pambano tu tafsiri yake yeye tayari ni bora na ana vigezo vya kuwania huo ubingwa.
kwahiyo mkanda uliwakutanisha mabondia ambao ni bora tayari.
"wakati PSG anakutana na Inter Milan fainali uefa wengi walikuwa na matokeo yao kabla lakini baada ya dakika 90 mshindi alionekana ni PSG walishinda kwa kishindo tu na aliwashangaza wadau wengi kwa kuonesha kiwango bora zaidi."
hata michel soro baada ya kumpiga hassan mwakinyo kwa TKO raundi ya 9 ameshangaza wadau wengi na alionesha mchezo mzuri sana.
ukiangalia sababu za mwakinyo kupoteza utaona tu alizidiwa mbinu pia alizidiwa nguvu hapo utapata jibu kwamba inabidi aboreshe zaidi mbinu zake na hata nguvu aongeze zaidi.
sasa vitu hivyo pekeake vinahitaji gharama kubwa ya kifedha na hassan pekeake hatoshi kabisa anahitaji kupewa ushirikiano mzuri.
ndomana awali nilisema kuna haja kubwa sana kwa mabondia kushikwa mkono maana sekta ya boxing ni pana sana na inahitaji uwekezaji.
nb: kwa wale ambao ni wazoefu wa mchezo wa boxing suala la wapiganaji kuongea maneno ya shombo ni jambo la kawaida sana.
kwasababu maneno ya shombo huwa ni sehemu ya mkakati wa kibiashara ili kujenga mvuto, kuongeza mauzo ya matangazo ya mapambano (Pay-Per-View), na kuingia kwenye akili za wapinzani wao ili kuwavuruga kisaikolojia.
kwahiyo hata hassan mwakinyo kutumia sana maneno ya shombo ni jambo la kawaida sana kwenye mchezo wa boxing labda uwe ni mgeni wa mchezo huo.
💁🏾♂️