Elcapitano Maestro

Elcapitano Maestro 1️⃣. Sports Pundit (English & Swahili) 2️⃣. i'm the best football analyst in africa

DARASA HURU 💁🏾‍♂️HASSAN MWAKINYO AMEPOTEZA PAMBANO RAUNDI YA 9 TKO DHIDI YA MICHEL SORO KUWANIA UBINGWA WA DUNIA IBO RAU...
11/06/2026

DARASA HURU 💁🏾‍♂️

HASSAN MWAKINYO AMEPOTEZA PAMBANO RAUNDI YA 9 TKO DHIDI YA MICHEL SORO KUWANIA UBINGWA WA DUNIA IBO RAUNDI 12.

Elcapitano Maestro 🗣 kuna haja kubwa sana kwa mabondia kushikwa mkono maana sekta ya boxing ni pana sana na inahitaji uwekezaji mkubwa.

mfano...serikali ya Marekani haitoi mchango wa kifedha au ruzuku yoyote ya moja kwa moja kwa mabondia wa nchi hiyo tofauti na mataifa mengine.

lakini marekani ni kitovu cha boxing kwasababu makampuni binafsi wamewekeza sana na kuifanya boxing kuwa biashara.

Mashirika ya Kibinafsi na Hisani: Mashirika k**a vile USA Boxing Foundation huchangisha fedha kusaidia gharama za kambi, vifaa, na masomo ya boxing.

hapo utagundua kwamba boxing ni zaidi ya mazoezi na ni zaidi ya kuwa nunda.

tathmini fupi pambano la mwakinyo dhidi ya michel soro...

mwakinyo alikuwa anagombea ubingwa wa dunia IBO, na kitendo cha kuwepo kwa hilo pambano tu tafsiri yake yeye tayari ni bora na ana vigezo vya kuwania huo ubingwa.

kwahiyo mkanda uliwakutanisha mabondia ambao ni bora tayari.

"wakati PSG anakutana na Inter Milan fainali uefa wengi walikuwa na matokeo yao kabla lakini baada ya dakika 90 mshindi alionekana ni PSG walishinda kwa kishindo tu na aliwashangaza wadau wengi kwa kuonesha kiwango bora zaidi."

hata michel soro baada ya kumpiga hassan mwakinyo kwa TKO raundi ya 9 ameshangaza wadau wengi na alionesha mchezo mzuri sana.

ukiangalia sababu za mwakinyo kupoteza utaona tu alizidiwa mbinu pia alizidiwa nguvu hapo utapata jibu kwamba inabidi aboreshe zaidi mbinu zake na hata nguvu aongeze zaidi.

sasa vitu hivyo pekeake vinahitaji gharama kubwa ya kifedha na hassan pekeake hatoshi kabisa anahitaji kupewa ushirikiano mzuri.

ndomana awali nilisema kuna haja kubwa sana kwa mabondia kushikwa mkono maana sekta ya boxing ni pana sana na inahitaji uwekezaji.

nb: kwa wale ambao ni wazoefu wa mchezo wa boxing suala la wapiganaji kuongea maneno ya shombo ni jambo la kawaida sana.

kwasababu maneno ya shombo huwa ni sehemu ya mkakati wa kibiashara ili kujenga mvuto, kuongeza mauzo ya matangazo ya mapambano (Pay-Per-View), na kuingia kwenye akili za wapinzani wao ili kuwavuruga kisaikolojia.

kwahiyo hata hassan mwakinyo kutumia sana maneno ya shombo ni jambo la kawaida sana kwenye mchezo wa boxing labda uwe ni mgeni wa mchezo huo.

💁🏾‍♂️

DARASA HURU 💁🏾‍♂️Rodrigo De Paul 🗣 Tutakwenda kuacha kila kitu chetu kwa muda huu kidogo kwa ajili ya Kombe la Dunia.Tun...
10/06/2026

DARASA HURU 💁🏾‍♂️

Rodrigo De Paul 🗣 Tutakwenda kuacha kila kitu chetu kwa muda huu kidogo kwa ajili ya Kombe la Dunia.

Tunatamani kuona ule muunganiko k**a ulio onekana 🇶🇦Qatar ukirudi tena.

Tunaweza kuondoka nalo kwa mara nyingine tena ya pili mfululizo"

💁🏾‍♂️

DARASA HURU 💁🏾‍♂️Nasser Al-Khelaifi (rais wa PSG) amesema kwamba 🗣 "Luis Enrique aliishi katika kituo chetu cha mazoezi ...
10/06/2026

DARASA HURU 💁🏾‍♂️

Nasser Al-Khelaifi (rais wa PSG) amesema kwamba 🗣 "Luis Enrique aliishi katika kituo chetu cha mazoezi kwa miezi 8 wala hakuenda nyumbani, alifanya kazi kuanzia saa 8 asubuhi hadi saa 3 usiku."

Tulimwomba atoke nje kwa muda, ili kubadilisha mazingira, lakini alikuwa amevutiwa sana na mchezo.

Maisha yake yote yamekuwa mpira wa miguu, tulianza hata kuogopa kwamba angepatwa na wazimu labda.

kwa bahati nzuri, tumeona matokeo ya bidii yake, kutoka kwake, wachezaji, usimamizi, na bila shaka mashabiki, imekuwa juhudi kubwa ya pamoja."

💁🏾‍♂️

DARASA HURU 💁🏾‍♂️Elcapitano Maestro 🗣Barcelona wanaamini Florentino Pérez aliwasilisha kimakusudi ofa ya €150M kwa Juliá...
10/06/2026

DARASA HURU 💁🏾‍♂️

Elcapitano Maestro 🗣Barcelona wanaamini Florentino Pérez aliwasilisha kimakusudi ofa ya €150M kwa Julián Alvarez ili kuongeza bei yake.

Hatua hiyo ilitoa mazingira bora kwa Real Madrid na Atlético...

Florentino Pérez anatimiza ahadi yake ya kampeni ya kutoa ofa ya €150 milioni huku Atlético ikiongeza bei yao ya kumuomba Julián Álvarez na kuimarisha msimamo wao wa mazungumzo na vilabu vingine...anasema Gaston Edul.

💁🏾‍♂️

DARASA HURU 💁🏾‍♂️Elcapitano Maestro 🗣 Real Madrid wapo sokoni kutafuta beki ambae atakuwa anacheza upande wa kushoto k**...
09/06/2026

DARASA HURU 💁🏾‍♂️

Elcapitano Maestro 🗣 Real Madrid wapo sokoni kutafuta beki ambae atakuwa anacheza upande wa kushoto k**a beki wa pembeni na awe na uwezo wa kucheza beki wa kati pale inapobidi.

Mabeki ambao wamependekezwa na real madrid ni pamoja na josko gvardiol na riccardo calafiori.

kabla ya kufikiria uamuzi huo wa madrid lazima kwanza tusifie jicho la arsenal na man city kwa kuweza kwenda na wakati.

kwa kawaida timu kubwa inakuwa na mechi nyingi katika msimu hivyo ni lazima uwe na wachezaji wenye uwezo mkubwa haswa katika eneo nyeti la ulinzi.

nb: kocha bora licha ya kuwa na uwezo mkubwa wa kufundisha pia ana jicho la usajiri mikel arteta ni moja ya makocha bora wa kizazi hiki cha leo.

💁🏾‍♂️

DARASA HURU 💁🏾‍♂️Elcapitano Maestro 🗣 ili bao liweze kupatikana kwa timu ya njano hapo ni nini kifanyike...?Je inabidi m...
09/06/2026

DARASA HURU 💁🏾‍♂️

Elcapitano Maestro 🗣 ili bao liweze kupatikana kwa timu ya njano hapo ni nini kifanyike...?

Je inabidi mwenye mpira hapo aupeleke wapi...? jaribu kufikiria mara mbili kisha majibu yako yapime na yangu.

🗣Mwenye mpira hapo tufanye ni X itabidi amchezeshe (ampasie) mchezaji asiekuwa na herufi ampe pass ambayo itayomfanya mchezaji pinzani (nyekundu) alazimike kujaribu kuufata mpira kisha mchezaji wa njano asiyekuwa na herufi akiukimbilia mpira akiupata ampasie herufi C wakati huo alieanza kuutoa mpira yule mchezaji X asogee juu haraka.

kisha herufi C ampasie herufi B kisha herufi B amrudishie mchezaji X ile pass ya kuomba one two (pass ya nipe nikupe).

hapo mchezaji X akimrudishia mchezaji B tafsri yake anaenda kukutana na golikipa na k**a mchezaji B atakuwa mzuri kwenye kufunga basi atafunga.

au k**a mchezaji A atakuwa na sifa ya kuweza kuvunja mitego ya kuotea hapo lazima mchezaji X atampasia mchezaji A ili kurahisisha kazi zaidi.

mbinu ya namna hio ☝️ hufanywa na timu chache sana ambazo zina washambuliaji wakali zaidi.

nb: mchezaji X...moja ya sifa ya kiungo mshambuliaji ni kujua ubora na udhaifu wa washambuliaji wake ni upi.

unapokuwa na kiungo mshambuliaji bora kwenye timu unakuwa na uhakika mkubwa sana wa kutengeneza nafasi za kufunga.

sasa je majibu yako yamekuwa k**a yangu au mtazamo wako ni upi...?

💁🏾‍♂️

DARASA HURU 💁🏾‍♂️Elcapitano Maestro 🗣 nimeona baadhi ya sehemu kwamba watangazaji wa media flani Tz wamekuwa na tatizo l...
09/06/2026

DARASA HURU 💁🏾‍♂️

Elcapitano Maestro 🗣 nimeona baadhi ya sehemu kwamba watangazaji wa media flani Tz wamekuwa na tatizo la kutolipwa mishahara kwa wakati.

Na bahati mbaya limekuwa ni tatizo sugu kwao, naona si katika busara watangazaji / mtangazaji kuanza kuvumisha habari kuhusu mishahara kwasababu kuna na sheria na taratibu ambazo anatakiwa azifate ili kupigania haki yake na si kwenda kinyume na hivyo.

🗣kuna baadhi ya media tz zilijaribu kutaka kufanya kazi na mimi lakini kwasababu mimi ndie mchambuzi bora zaidi wa soka barani Afrika kuna gharama kuwa na mimi na niliwaambia.

ukiwa na Elcapitano Maestro hutapata uchambuzi tu bali hata ushauri wa namna ya kuwa na kipindi bora cha michezo tofauti na wengine.

💁🏾‍♂️

DARASA HURU 💁🏾‍♂️Kvaratskhelia (kwenye fainali ya UCL dhidi ya Inter)...psg 5 - 0 inter milan.Kvaratskhelia 🗣"Nilijua mt...
09/06/2026

DARASA HURU 💁🏾‍♂️

Kvaratskhelia (kwenye fainali ya UCL dhidi ya Inter)...psg 5 - 0 inter milan.

Kvaratskhelia 🗣"Nilijua mtindo wa uchezaji wa Inter kwa sababu nilikuwa nimewakabili mara kadhaa.

Kushinda dhidi yao haikuwa rahis hata kidogo kwasababu wana nguvu sana katika ulinzi na pia kwenye counter na kwenye mipira ya kutengwa kwa hakika Ilibidi uwe tayari kupigana na kubaki makini sana wakati wote.

kuelekea fainali dhidi ya inter milan tulijifunza kitu kupitia barcelona, naamini sababu kuu iliyopelekea sisi kushinda 5-0 ni kwamba hatukuacha kushambulia dhidi yao."

💁🏾‍♂️

DARASA HURU 💁🏾‍♂️TIMU YA UHISPANIA(SPAIN) WATABEBA UBINGWA WA KOMBE LA DUNIA 2026.Elcapitano Maestro 🗣 kile kilichoanzis...
08/06/2026

DARASA HURU 💁🏾‍♂️

TIMU YA UHISPANIA(SPAIN) WATABEBA UBINGWA WA KOMBE LA DUNIA 2026.

Elcapitano Maestro 🗣 kile kilichoanzishwa na Luis de la fuente katika timu ya taifa ya uhispania kitaenda kukamilishwa awamu hii kwa timu hio kubeba ubingwa wa kombe la dunia 2026.

Mpira wa miguu ili uwe mshindi haikuhitaji tu uwe na wachezaji nyota zaidi bali utatakiwa pia uwe na wachezaji ambao wataweza kupambana kwa ajiri ya timu.

timu ya uhispania ina aina yake ya uchezaji pia uwepo wa mchezaji bora yamal ni moja ya faida kubwa sana kwao.

Luis de la fuente ni kocha ninae muamini sana sitategemea kuona akirudia makosa aliyofanya hansi flick kwa kumuacha yamal ndio awe kila kitu uwanjani.

ikiwa atashindwa kujifunza kupitia hans flick nitasikitika kwasababu fuente atashindwa kubeba ubingwa na utabiri wangu utapotea kwa mara ya kwanza.

💁🏾‍♂️

DARASA HURU 💁🏾‍♂️Elcapitano Maestro 🗣 Gazeti la Ufaransa la L'Equipe linaripoti kwamba Ousmane Dembele anajiona k**a mmo...
08/06/2026

DARASA HURU 💁🏾‍♂️

Elcapitano Maestro 🗣 Gazeti la Ufaransa la L'Equipe linaripoti kwamba Ousmane Dembele anajiona k**a mmoja wa viongozi katika timu ya taifa ya Ufaransa.

Mshindi mara mbili wa Ligi ya Mabingwa na mshindi wa Ballon d'Or, alionekana akimwambia Mbappe ajue namna ya kuisaidia timu kwenye ulinzi na aongeze kasi yake uwanjani.

💁🏾‍♂️

Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255620587262

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Elcapitano Maestro posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Elcapitano Maestro:

Share

Category