04/01/2026
Mwamuzi Boubou Traore kutoka Mali ameikosesha Taifa Stars fursa ya kupata bao la kusawazisha kupitia mkwaju wa penalti baada ya 'kumeza filimbi' pale ilipobidi kutoa adhabu baada ya mshambuliaji wa Stars, Iddi Nado kusukumwa ndani ya 'box' la Morocco dakika za jioni kabisa wakati wenyeji hao wakiwa mbele 1-0.
Licha ya shinikizo kutoka kwa wachezaji na benchi la ufundi la Taifa Stars wakimtaka REFA huyo akaangalie tukio hilo kwenye VAR, lakini Mwamuzi 'Bubu' aliendelea kuwa bubu na kuendeleza mchezo huo uliomalizika kwa Stars kutolewa isivyo haki.
Tukio lile Duniani kote ni 'tuta' la wazi kabisa lakini Boubou Traore aliamua kulifumbia macho tena mbele ya Rais wa CAF, Patrice Motsepe na Rais wa FIFA, Gianni Infantino waliokuwepo katika dimba la Prince Moulay Abdellah mjini Rabat kushuhudia mtanange huo.