05/06/2026
Mabondia wa Ngumi za Kulipwa nchini Lulu Kayage a.k.a 'Anaconda' na mpinzani wake Jennifer Bernard Sige a.k.a 'Jennifer Zugo' almaarufu 'Kiboko Ya Warembo' Tarehe 27/06/2026 wanatarajia kupanda ulingoni kwenye mapambano makali ya Usiku wa Vyuma Vitaumana.
Kayage na Jennifer watacheza pambano la raundi 6 za Moto kwenye uzani wa Super Bantamweight kg 44 lililoandaliwa na Mitra Boxing Promotion huku likifanyika kwenye ukumbi wa Heinken Mtoni Kijichi jijini Dar es Salaam.
Hili ni pambano lenye mvuto zaidii lenye Heshima na Kisasi ndani yake upande wa Kayage ni bondia mkongwe aliyeingia kwenye mchezo huu tangu mwaka 2017 mwenye uzoefu wakutosha aliyewahii kushea ulingo mmoja dhidi ya mabondia mashughuli kwenye upande wa ngumi za kulipwa kwa Wanawake k**a Stumai Muki, Jesca Mfinanga, Halima Vunjabei n.k huku akicheza mapambano kadhaa ya kimataifa nnje ya mipaka ya Tanzania.
Jennifer ni bondia damu changa anayechipkia kwenye mchezo huu anaesimamiwa na Zugo Boxing Gym chini ya kocha wake Selemani Zugo na hapa kuna kisasi ndani yake kwani itakumbukwa bondia Kayage alishawahii kuwa chini ya mikono ya kocha Zugo kabla ya kutengana kwao na kwa kipindi cha miaka kadhaa bondia huyo amewahii kuwapiga mabondia wengi kutoka kwa kocha wake huyo na safari hii anaenda kukutana na kiboko ya Warembo Jennifer miongoni mwamabondia wakali wanaokuja nakufanya vizuri kwenye mchezo huu.
Kiufundi kiuchezaji Kayage na Jennifer wote ni mabondia wanaocheza upande sawa wa kushoto (Orthodox) kwenye kutanguliza miguu yao ya mbele na kiasili Kayage ni bondia ambaye ni Pure Fighter mwenye kucheza mfumo wakufuata nakupigana na Jennifer ni bondia ambaye ni Boxer mwenye kucheza mfumo waku Box ndani ya ulingo huku akifanya mitembeo na kuweka gepu la nafasi kwa ajili ya score point's za ushindi.
Kayage ana Total Fight's 27, Win's 8, 'KO'S' 2, Lose 15 Draw 4.
Jennifer ana Total Fight's 2, Win's 1, 'KO'S' 1, Lose 0 Draw 1.
June 27 hapa Anaconda pale Kiboko ya Warembo unipe heshima yangu au niichukue kwa nguvu tukutane ndani ya Mtoni Kijichi tukaone mikono ikisema usikose familia.
Mn Boxing Media Tanzania