25/08/2026
Moja kati ya vitu vinavyowavutia mashabiki wengi wa mchezo wa Masumbwi ni matokeo ya Knockout (K.O) na Technical Knockout (TKO) hasa pale mpambano unapofikia hatua ambayo mmoja kati ya wapinzani wawili anaanguka na kulamba sakafu ya ulingo (Canvas).
Kwa kipindi cha miaka mingi katika tasnia ya mchezo wa Masumbwi hapa nyumbani, mashabiki wamepata kushuhudia mapambano mbalimbali yaliyomalizika kwa Knockout za kutisha, huku baadhi yake yakiwaacha mashabiki wakishikilia vichwa kutokana na ukubwa wa pigo lililomaliza pambano.
Na kwa kweli, k**a si mipango ya Mungu, huenda baadhi ya mabondia waliowahi kuanguka kwenye mapambano hayo tusingekuwa tunawaona leo.
Hapa nimekuletea baadhi tu ya mapambano yaliyomalizika kwa K.O / TKO hatari yaliyowahi kufanyika hapa nyumbani, k**a yanavyoonekana kwenye mpangalio wa video clips hapo chini :
1️⃣ Ibrahim Class 🆚 Gustavo Pina Melgar raia wa Mexico 🇲🇽
📅 30/09/2022
Class alishinda kwa K.O raundi ya 9 kati ya 10.
2️⃣ Joseph Maigwisya 🆚 Hussein Itaba
📅 15/07/2023
Maigwisya alishinda kwa K.O raundi ya 5 kati ya 6.
3️⃣ Juma Choki 🆚 Salim Chazama raia wa Malawi 🇲🇼
📅 26/12/2021
Choki alishinda kwa K.O raundi ya 3 kati ya 6.
4️⃣ Ramadhani Iddi “Bonnie Sellah” 🆚 Ramadhani Kondo
📅 22/10/2023
Bonnie alishinda kwa K.O raundi ya 1 kati ya 8.
5️⃣ Allan Kamote 🆚 Twalibu Mchanjo
📅 31/01/2020
Kamote alishinda kwa K.O raundi ya 4 kati ya 8.
6️⃣ Ally Sewe Jr 🆚 Mohammed Mnemwa
📅 24/01/2025
Sewe Jr alishinda kwa K.O raundi ya 1 kati ya 4.
7️⃣ Ramadhani Mkwakwate 🆚 Isack Chaka
📅 30/08/2025
Mkwakwate alishinda kwa K.O raundi ya 1 kati ya 8.
8️⃣ Amani Bariki 🆚 Hemed Habibu
📅 20/11/2022
Bariki alishinda kwa TKO raundi ya 8 kati ya 8.
9️⃣ Dullah Mbabe 🆚 Francis Cheka
📅 26/12/2018
Dullah Mbabe alishinda kwa K.O raundi ya 6 kati ya 8.
Hizo ni baadhi tu ya Knockout za Hatari zilizowahi kutokea kwenye ulingo kupitia mapambano yaliyofanyika hapa nyumbani.
Je kati ya hizo Knockout 9, ipi unaihesabu kuwa ilikuwa K.O/TKO kali zaidi? Au kuna Knockout nyingine hatari ambayo unadhani ilipaswa kuwepo kwenye orodha hii shusha comment yako familia.
Mn Boxing Media Tanzania