15/01/2022
π¨RATIBA
Timu ya Wananchi Yanga imefika salama mkoani Tanga tayari kwa mchezo dhidi ya Coastal union siku ya jumapili tarehe 16.1.2022 mchezo utakaopigwa kwenye dimba la mkwakwani.
Yanga imefika Tanga na wachezaji wao wote isipokuwa wachezaji watatu ambao ni majeruhi hawapo Tanga nao Ni pamoja na;
π° Yacouba songne (Yupo Tunisia amekwenda kuonana na Daktari kwa ajiri ya maendeleo ya jeraha lake ambalo alifanyiwa upasuaji mdogo wa goti la kulia)
π° Kibwana shomari (Yupo Tunisia kwa matibabu)
π° Abdallah shaibu Ninja (Yupo Tunisia kwa matibabu)
Wachezaji wengine wote pamoja na benchi la ufundi likiongozwa na Kocha Nabi lipo Tanga tayari kwa maandalizi ya mwisho kabla ya mchezo hapo kesho.
YANGA KUCHEZA MCHEZO WA KIRAFIKI ARUSHA JUMATANO DHIDI YA MBUNI FC UWANJA WA SHEKHE AMRI ABEID.
Timu ya Wananchi Yanga itaanza safari ya kwenda Mkoani Arusha siku ya jumatatu Asubuhi tarahe 17.1.2022 na baadae yaani jumatano ya tarehe 19.1.2022 Timu ya Wananchi Yanga watacheza mchezo wa kirafiki na MBUNI FC mchezo wa kirafiki kwenye dimba la Shekhe Amri Abeid kuanzia majira ya saa 10:00 jioni.
Mara baaada ya mchezo wa kirafiki Yanga wataanza tena safari ya kuwafuata wenyeji wao Police Tanzania.Mechi Kati ya Police Tanzania na Yanga itachezwa tarehe 23.1.2022 kwenye dimba la Ushirika.
All ze best timu ya Wananchi Yanga π’π‘πͺππ