28/09/2022
2002 fainali za Kombe la Dunia kati ya Ujerumani na Brazil iliwekwa k**ari matata sana, huku German wakijivunia golikipa wao mashuhuri kwelikweli Oliver Kahn na huku Brazil wakijivunia mshambuliaji wao hatari kabisa Ronaldo De Lima.
Ikawa ni majivuno kati ya Oliver Kahn na Ronaldo De Lima. Kahn aliapa kamwe hatafungwa na Ronaldo katika fainali ni bora afungwe na mchezaji mwingine lakini sio Ronaldo. Ronaldo nae aliapia kuwa atamfunga Kahn kuanzia mabao mawili na kuendelea na k**a atafunga bao moja Basi atatoa nyumba zake na magari yake yoote ya kifahari kwa Oliver Kahn.
Kufkia mapumziko ubao unasoma 0-0 wachezaji wa Ujerumani walipongezana kwa kumdhibiti Ronaldo. Hakupiga shuti hata moja. Kipindi cha pili kilianza mpaka kufkia dakika ya 60 hakuna timu iliyoona lango la mwenzake. Hapo Kahn akaanza kejeli "zimebaki dk 30 tu unipe Mali zangu" Ronaldo akajibu "Mpira unaingia wavuni kwa sekunde moja tu, nna sekunde zaidi ya 1800"
Ikawa dakika ya 67, Ronaldo akafunga bao kali. Oliver Kahn alipiga kelele kwa mabeki zake kumuachia nafasi mshambuliaji k**a Ronaldo kupiga anavyotaka. Haikutosha dakika ya 79 Ronaldo anaingia tena kambani baada ya Rivaldo kuuacha mpira umpite tobo ndani ya 18 akijua wazi utamfkia Ronaldo ambae nae bila kujiuliza aliutungua kisawasawa ukazama wavuni, ubao ukasomeka 0-2. Oliver Kahn alilala baada ya bao la pili alilia sana. Baada ya mechi kuisha alisema:
"Dunia ina wachezaji lakini Ronaldo ni Dunia nyingine". Watu wengi waliipa ushindi German kutokana na ubora wa Oliver Kahn ambae alipewa jina na kuitwa kipa wa Dunia haikua easy kumfunga. Lakini alisarenda kwa Ronaldo De Lima.
Kuna magolikipa wengine wengi tu huwa wanakataa kufungwa na flani. Gigi Buffon robo fainali ya Uefa 2017 kati ya Juventus na Monaco alisema anaheshimu uwepo wa kinda Kylian Mbappe lakini kumfunga hawezi. Dakika ya 69 Mbappe anamfunga Buffon na Buffon anaenda kumbusu Mbappe kichwani kukubali japo Monaco walitolewa kwa agg ya 4-1.
Follow: Soka Viwanjani 💥