13/05/2015
Michezo ni sehemu muhimu sana katika utamaduni wa kila jamii ya binadamu duniani kote. Kila kipindi cha historia ya binadamu kinaonyesha jinsi binadamu alicyobuni na kuendeleza michezo kulingana na mazingira yake ya kisiasa, kiuchumi na kijamii. Kutokana na mabadiliko ya mazingira hayo michezo iliyochezwa na jamii ilikuwa inabadilika mara kwa mara. Baadhi ya mabadiliko hayo ni pamoja na hali ya mchezo, sheria na kanuni ili kukidhi mabadiliko hayo.
Tanzania k**a jamii tulikuwa tukishiriki katika michezo mbalimbali katika kabila zetu. Tulishiriki katika michezo ya mieleka, kutupa mkuki, kulenga shabaha kwa upinde na michale, sarakasi, kukimbia, kuruka, kuogelea, kucheza bao n.k.
Madhumuni ya michezo hii yalikuwa ni:-
i) Kutoa burudani kwa jamii baada ya kazi;
ii) Kujenga na kukomaza afya ya mwili na akili;
iii) Kujenga ukak**avu, nidhamu na uwezo wa kujihami kwa mtu binafsi na kwa jamii;
iv) Kuonyesha uwezo na vipaji vya washiriki na kutangaza hulka ya jamii kwa jamii nyingine;
v) Kuwa kiungo baina ya jamii mbalimbali;
vi) Kukuza na kuendeleza uhusiano wa kirafiki baina ya jamii mbalimbali.
Katika mazingira ya kikabila k**a yalivyokuwa katika jamii nyingi, Kanuni za mfumo wa kikabila zilitawala uendeshaji wa shughuli za michezo.
Kuingia kwa wageni na wakoloni nchini mwetu kuliambatana na kuingizwa kwa michezo ya kigeni k**a Mpira wa miguu, Hoki, Ndondi, n.k. Mchezo wa Riadha ambao ulikuwa ukichezwa katika jamii zetu nyingi kabla ya ujio wa wageni hawa, uliletwa katika sura mpya ya kisasa na inayotambulika Kimataifa, Kadri nchi yetu ilivyozidi kuingia katika ulingo wa Kimataifa ndivyo michezo mingi zaidi ilivyoingia nchini na kuimarika. Michezo k**a Mpira wa Miguu, Mpira wa Kikapu, Mpira wa Wavu, Tennis, Mpira wa Meza, Mpira wa Mikono, Kriketi, Golf, Baiskeli na kadhalika, kila mmoja uliweza kujipatia umaaarufu kulingana na wakati.
Pamoja na kwamba michezo ya kigeni ilisaidia sana kufanya