12/06/2026
Nahodha na kipa wa timu ya taifa ya Afrika Kusini, Ronwen Williams, ameeleza masikitiko yake kufuatia kile alichokitaja kuwa ukosefu wa mshik**ano kutoka kwa baadhi ya mataifa ya Afrika wakati wa mchezo wa ufunguzi wa Kombe la Dunia 2026 dhidi ya Mexico.
Williams alisema kuwa yeye na wenzake walikuwa na matarajio makubwa ya kupata sapoti kutoka kwa Waafrika wengi k**a wawakilishi wa bara hilo katika mashindano hayo. Hata hivyo, alidai kushangazwa na hali ya baadhi ya mashabiki wa Afrika kuonekana kuiunga mkono Mexico katika mchezo huo uliomalizika kwa ushindi wa mabao 2-0 kwa upande wa Mexico.
“Tulitarajia bara letu lingesimama nasi katika nyakati k**a hizi, lakini haikuwa hivyo. Hilo lilikuwa la kusikitisha,” alisema Williams.
Kipa huyo aliongeza kuwa aliona mashabiki wengi kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika wakiwa wamevalia jezi za Mexico wakati wa mchezo huo, jambo alilolitafsiri k**a ishara ya kuipa sapoti timu pinzani badala ya kuiunga mkono Afrika Kusini.
Kauli za Williams zimeibua mjadala miongoni mwa wadau wa soka kuhusu umuhimu wa mshik**ano wa bara la Afrika katika mashindano makubwa ya kimataifa, hususan pale timu za Afrika zinapokuwa zikiwakilisha bara hilo dhidi ya mataifa kutoka mabara mengine.