21/05/2026
MIKEL ARTETA ANAVYOYAISHI KWENYE NDOTO ZA DAVID DEIN -02.
Jioni moja akiwa kwenye msongo wa mawazo kuhusu Arsenal inaongezaje uchumi wake, David Dein aliwaza kuhusu anavyoweza kuwatumia mashabiki kuongeza kipato, lakini atafanya kwa mtindo gani, ndiyo swali kubwa kwake.
Alimuita mwanahisa mwenzake Peter Hill-Wood akamueleza dhamira ya kuhama uwanja wa Highbury kwakua hakuna option ya kufanya upanuzi kutokana na mazingira ya North London na kisheria, wakati Peter anapokea wazo kwa Mastermind na Chairman wa wakati huo, David akaendelea.
Arsenal inatakiwa kubadilika kutoka Traditional football Club mpaka Morden Global Financial, kubadilisha utamaduni wa soka kuanzia, Sayansi ya mpira, Nutrition kwa wachezaji, Identification ya playing style, David alihisi tunapaswa kuwa MODERNISATION CLUB kwenye soka.
Wazo la Arsene Wenger likaingia...
Wakati huo alikua anaondoka kocha hodari, Mr. Chapman, David alimwambia Hill-Wood, kuna mfaransa mmoja yupo ligi ya Japan yule ni FUTURE OF FOOTBALL, anatufaa kwenye mabadiliko yetu, Hill-Wood akamuuliza, tunamletaje UNKNOWN FRENCHMAN, tena kutoka ligi ya Japan, upo serious kweli?
David hakumpinga mwanahisa mwenzake, akaletwa kocha ambaye hakufanikiwa, walivyomfukuza, akamwambia wazo langu ni lilelile kuhusu Arsene Wenger, 1996, anaingia Wenger na kulindwa kwenye Media.
Migogoro ilivyoanza kuleta migawanyiko na Arsenal kuanza kushuka ( Why Arsenal decline ).
Baada ya ujio wa Arsene waliingia mastaa wakubwa k**a THIERY HENRY, DENIS BERGKAMP, IAN WRITE, akabeba mataji ikiwemo The Invisible, kumbuka kipindi hicho bado klabu inamilikiwa na Old Arsenal families, hakuna kibosile.
Arsenal walianza mchakato wa kuhama dimba la Highbury mpaka ASHBURTON GROVE ( Emirates Stadium ), haikuwa project nyepesi, zaidi ya euro milioni 600 ziliwekezwa kupitia mikopo ya Banks, Bonds, Future Stadium Revenues, hatimae uwanja ulikamilika mwaka 2006.
Kutokana na madeni mengi kuielemea Arsenal, kocha aliyepigania dimba hilo ili kuongeza uchumi wa klabu, Bw. Wenger, alianza kutumia uchumi wake kwa kuuza mastaa k**a Samir Nasri, Robin Van Persie, Cecs Fabregas.
Tunatakiwa kuleta wawekezaji wapya ili kuingia kwenye ushindani, ilikua kauli....