15/09/2022
Mathias Pogba (32) ambaye ni kaka wa nyota wa Juventus Paul Pogba (29) anashikiliwa na Polisi kuhusiana kula njama akiwa na rafiki zake na kutaka kumuibia mdogo wake Paul
Kiungo huyo wa zamani wa Manchester United alidai mwezi uliopita kuwa alikuwa muathirika wa njama ya pauni milioni 11 iliyokuwa ikipangwa na marafiki zake wa utotoni pamoja na kaka yake.
Kwa mujibu wa gazeti la Le Monde Mathias alijisalimisha mwenyewe kwa Polisi wa Ufaransa wanaofanya uchunguzi wa kesi hiyo.