21/11/2025
KUSEMA UKWELI SIO DHAMBI BALI NI UKOMAVU...
"Nikiwa zangu huku mbali bado ninafuatilia mijadala kuhusiana na Jezi za kimataifa kwa timu zetu pendwa na pasua kichwa hapo Bongo..
Ni ukweli usiopingika kuwa siku za karibuni kumekuwa na utamaduni wa kuzindua jezi katika awamu mbili endapo timu itafuzu kucheza hatua ya makundi katika michuano ya Afrika iwe klabu Bingwa au kombe la Shirikisho..
Yanga walianza na kutangaza watazindua siku ya Jumatano huku Simba wao wakizindua Alhamis hii.
Achana na ubora au nani katoa jezi kali ni kawaida kuona ushindani uliojaa utani ndani yake lakini hili la kuzindua jezi ile ile na kuamua kubadili logo na wadhamini halipo sawa na haliwezi kupata utetezi wa kiwango cha lami kutoka kwa wazee wa kutembelea fursa kwani kufanya hivyo ni kujichoresha na kujipunguzia hadhi kuliko pitiliza.
Nimeona watu wakijaribu kuhamisha upepo eti Mdhamini aliyepo huwa anatoa jezi moja tu kwa msimu! Haya tufanye ni sawa, sasa kwanini mlitangaza kutakuwa na uzinduzi wa Jezi za Michuano ya kimataifa? Au ni uzinduzi wa Nembo ya CAF kukaa begani na kumtoa Mdhamini wa awali na kuweka mpya? is it serious?
Mliposema wafanyabiashara waweke order mlisahau kuwa jezi ni zile zile ambazo bado zipo madukani zikisota kununuliwa?
Sasa fikiria mtu alikuwa na mzigo wa mwanzo ambao haujakata na tayari umemtangazia alipie mzigo mpya, analipia kumbe unaenda kumuongezea mzigo ule ule ambao anapambana nao kuumaliza walao arudishe pesa ya mtaji,Je kwa hili ni sawa? na bado wapo wanaotetea hili haumuoni mnategeneza mahusiano mabaya na kupoteza kuaminika kutoka kwa wateja wenu wa jezi za jumla.?
Ngoja niwaambie kitu sio kila wakati ni kutafuta pa kujifichia wakati mwingine kuweni wakweli ili k**a kuna changamoto mzitatue ili timu isonge mbele na kwa wale mnaoendekeza maelekezo kwa kujipatia ujira jitahidini kuwaza na kesho kwani njaa ipo tu haiishi mpaka siku tunarudi kwa aliyetuumba..
Katika hili mmepuyanga sana ni vema mkatoka na kuomba radhi kwa wafanyabiashara,mashabiki wenu na wadau wote wa Soka."
Ameandika Mchambuzi wa soka kupitia ukurasa wake wa Instagram