10/06/2026
Liverpool imeanza kuongeza juhudi kumsajili beki wa kulia chipukizi wa Italia, Marco Palestra kutoka Atalanta.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka England, Liverpool wameongeza kasi ya kumfuatilia mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21, ambaye kwa sasa yuko kwa mkopo katika Cagliari akitokea Atalanta.
Palestra anatajwa k**a mmoja wa vipaji vinavyopanda kwa kasi Serie A kutokana na uwezo wake wa kuzuia na kusaidia mashambulizi upande wa kulia, jambo linalomfanya aonekane k**a chaguo la muda mrefu kwa klabu kubwa Ulaya.
Kwa sasa hana nafasi ya kudumu kikosi cha kwanza Atalanta, hali inayoweza kufungua mlango wa uhamisho kwenda Liverpool endapo makubaliano yatakamilika.
Source: BE SSOCCER
Follow Football kitaa, @ Eddywizzyboetz.