20/07/2026
Simba SC imefungua vizuri dirisha la usajili kwa kuanza kuwatambulisha wachezaji Kelvin Nashon (Kiungo Mkabaji) na Nathan Chilambo (Beki wa kulia)
Kitu kizuri ni kuwa wachezaji hawa wote wawili wana uzoefu mkubwa wa ligi kuu ya NBC na wana uwezo wa kukabiliana na presha ya michezo mikubwa jambo ambalo wameshathibitisha kwenye vilabu walivyotokea.
Chilambo anakuja kuimarisha safu ya ulinzi ya Mnyama hasa upande wa kulia ambao ulikuwa na machaguo mawili tu Shomari Kapombe na David Kameta ambapo mara kadhaa yalionekana madhaifu madogo madogo kwenye eneo hilo lakini ujio wa Chilambo utaenda kuamsha hari na ushindani kwenye eneo hilo na kufanya mbavu ya kulia ya Mnyama Simba iwe imara zaidi.
Kelvin Nashon ambaye ni kiungo mkabaji mwenye uzoefu mkubwa wa kutawala eneo la chini la kiungo anakuja Msimbazi kuongeza uimara katika eneo hilo ambalo tayari lina watu mahiri k**a Yusuph Kagoma na kijana Hussein Semfuko, hakuna asiyefahamu ubora wa Kelvin Nashon kwenye vilabu vyote alivyopita na sasa ni wakati wa kudhihirisha ubora wake kwenye jukwaa kubwa la Mnyama Simba.
Simba SC bado wanashusha vyuma lakini hizi karata walizoanza nazo zinaonesha ni kwa namna gani viongozi wa Simba SC walitulia sokoni ili kuwaletea Wanasimba wachezaji wenye quality inayoendana na timu yao.
MNYAMA YUPO SERIOUS SANA π¦π₯