12/12/2025
Afisa habari na mawasiliano wa Shirikisho la Mpira Tanzania TFF Clifford Mario Ndimbo amesema malengo ya Tanzania kwenye mashindano ya AFCON 2025 mwaka huu ni kuchukua kombe.
Ameyasema hayo Leo Disemba 12 akizungumza na waandishi wa habari ambapo amesisitiza kwamba lengo kuu ni Kombe mambo yasipokuwa mazuri basi tufike kwenye hatua za mtoano.