05/09/2026
🚨Klabu ya Yanga imefanikiwa kupata sare ya bao (1-1) kwenye mchezo wake wa raundi ya kwanza hatua ya awali Ligi ya Mabingwa barani Afrika (CAF Champions League 2026/27) mbele ya Gaborone United wakiwa ugenini nchini Botswana.
➡️Bao la kusawazisha limefungwa na Seleman Mwalimu dakika ya 90+6 na kuisaidia Yanga kupata sare hiyo.
➡️Mchezo wa marudiano unatarajiwa kuchezwa Septemba 12,2026 kwenye dimba la Azam Complex jijini Dar Es Salaam.
➡️Ili Yanga wafanikiwe kusonga mbele lazima wapate ushindi wa bao moja au zaidi.
NB: Je Yanga itafanikiwa kuiondosha Gaborone United?