11/04/2026
Nilituma kimakosa 200K kwa nambari isiyo sahihi.
Baada ya kuwaza namna ya kumzuia asitoe hizo pesa, nikapata idea ya kumtumia SMS nikisema:
“Sasa dark initiate mwenye umechaguliwa, natumai uko poa. Naam, naamini umepokea pesa nilizokutumia…
Hizo ni za transport ya initiation yako ya kujiunga na Illuminati pamoja na order ya satanism ya milele, inayofanyika kesho saa sita usiku. Hiyo pesa ni fare tu.
Nitakutumia ingine ya shopping. Kuna utajiri mkubwa unakusubiri kwa huu ufalme. Wiki mbili baada ya initiation, mtu wa familia ambaye uko karibu naye sana atakufa, na hiyo ndiyo itafungua mlango wa utajiri wako. Pia utakuwa na uwezo wa kuruka usiku kwenda popote duniani. Asante mapema.
Lakini k**a bado hujakuwa tayari kujiunga, tafadhali rudisha pesa mara moja ili kuepuka kifo cha ghafla.”
Dakika tano baadaye nikapata SMS ikisema:
“Tuma 600k ingine, marafiki zangu watatu pia wako interested.” 😭😂😂
WALAI HII IMEENDA